IAA, TAKUKURU ZAENDESHASEMINA YA MAADILI KWA WAFANYAKAZI NA WAADHIRI WA CHUO CHA UHASIBU

 Chuo cha Uhasibu Arusha kwa kushirikiana na Taasisi ya kupambana na Rushwa(Takukuru)Mkoa wa Arusha imeendesha semina ya maadili kwa wafanyakazi na wahadhiri Chuoni hapo kutambua namna bora ya kupambana na Rushwa


Akizungumza katika semina hiyo Afisa uchunguzi kutoka Takukuru Salum Nyangwese ambaye alikuwa mtoa mada alisema kuwa mazingira ya rushwa hutengenezwa na wafanyakazi wasio na maadili kazini

Kwa upande wake mwanasheria wa Takukuru Violet Machery amewataka wafanyakazi hao kuzingatia mafunzo hayo ili kufanya kazi kwa weledi na umakini katika utekelezaji wa majukumu yao

Wanufaika wa semina hiyo walishukuru kwa uwepo wa mafunzo hayo ambayo yatawajengea uwezo na uelewa mkubwa katika kutambua vitendo vya rushwa

Lengo la semina hiyo ni kuboresha utendaji kazi pamoja na watumishi kufata maadili ya utumishi wa Umma.
Mwanasheria wa Takukuru Violet Machery akitoa mada katika Chuo cha uhasibu Arusha.
Afisa Uchunguzi kutoka Takukuru Mkoa wa Arusha Salum Nyangwese akitoa mada

Wafanyakazi wa uhasibu Arusha wakifatilia mada mbalimbali

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

Previous Post Next Post