BREAKING NEWS

Thursday, March 17, 2022

WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA WATUMIE KALAMU KUISEMEA VYEMA SERIKALI

meneja wa Uhifadhi wa taarifa na machapisho kutoka Tume ya taifa ya sayansi na Teknolojia  Dr.Wilbert Bunini akimkabidhi mwandishi wa habari  kutoka daily news Edward Koro cheti  Cha ushiriki wa mafunzo ya siku nne yaliolenga kuwajengea uwezo wa kuandika habari za tafiti mbalimbali zinazotolewa na wanasayansi na kuzifikisha kwa wananchi kwa lugha rahisi mafunzo yaliyoandaliwa na  na tume hiyo Kwa uthamini wa serikali yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo katika jengo la mkuu wa mkoa wa Arusha kulia ni  Kaimu Mkurugenzi wa  Tume ya sayansi na Teknolojia (COSTECH) Dk. Philbert Luhunga  (picha na Woinde Shizza)
 


Na Woinde Shizza , ARUSHA


Waandishi wa habari wametakiwa watumie kalamu zao kuisemea vyema nchi yao pamoja na serikali Kwa ujumla huku Ili kuendelea kuilinda amani ya nchi 



Hayo yamebainishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Tume ya sayansi na Teknolojia (COSTECH) Dk. Philbert Luhunga alipokuwa akiongea na waandishi wa habari wa mikoa ya Arusha , Kilimanjaro na Manyara katika mafunzo ya siku nne yaliolenga kuwajengea uwezo wa kuandika habari za tafiti mbalimbali zinazotolewa na wanasayansi na kuzifikisha kwa wananchi kwa lugha rahisi yaliyoandaliwa na tume hiyo Kwa uthamini wa serikali .



Alisema kuwa katika kufanya kazi zao ni vyema waandishi wa habari wajiheshimu ,wajitambue pamoja na kufanya kazi Kwa weledi wa hali ya juu huku wakiweka mbele maslahi ya nchi yao.


Alisema kuwa lengo la kuandaa mafunzo hayo Kwa wanahabari ni kuwaelimisha zaidi na kuwajengea uwezo mzuri wa kuandika habari za tafiti mbalimbali zinazofanywa na wanasayansi wetu na kuzifikisha Kwa Wananchi Kwa lugha rahisi ambayo itamuwezesha mwananchi wa kawaida kuielewa vyema.



"watafiti wamekuwa wanafanya tafiti mbalimbali baada ya hapo wanaandika taarifa za tafiti walizofanya kwa lugha ambazo si rafiki jambo ambalo wanapopelekewa taarifa hizo wanashidwa kuzifanyia kazi wengine hawaelewi kutoka ana lugha ambazo watafiti hao wamekuwa wanazitumia hivyo ndio maana tumewaita nyie mjifunze Ili tafiti hizi mkizipata muandike kwa lugha nyepesi ambayo itamuwezesha mwananchi kuelewa"alisema



Kwa upande wake mkufunzi wa mafunzo hayo Dkt Baraka Msangi alisema kuwa tafiti hiI zikiandikwa kwa lugha rahisi na zikawafikia wananchi itawasaidia kufanya maamuzi katika kutatua yao ya kila siku


Aidha aliwataka watafi hao kuandika machapisho yao kwa ufupi ili kuweza kumrahisishia mwananchi kusoma na kuelewa kiuraisi

. ikiwemo dawa za kutibu magonjwa ya wanawake ,dawa za kutibu magonjwa ya ngozi ,dawa za kutibu magonjwa ya macho pamoja na dawa ya ugonjwa wa uzio.


Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates