BREAKING NEWS

Monday, March 21, 2022

MKE MTARAJIWA WA LYATONG A MREMA AVUNJA UKIMNYA



 Kutokana na kuwepo kwa taarifa mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii kuhusiana na Mwenyekiti wa Tlp Taifa Augostino Mrema ,hatimaye Mkewe Halima amevunja ukimya kuhusu ndoa yake na Mwenyekiti huyo.


Kwamba hana ugomvi na familia yake na watu waache uzushi wa kumzushia kwamba mumewe huyo mtarajiwa amepata upinzani mkubwa kumuoa yeye .

Amesema kuwa,hana mgogoro wowote na mpenzi wake mtarajiwa wananchi wapuuze maneno yanayosambazwa mtandaoni kwamba yeye na mzee wana mgogoro sio kweli,

Bali familia wanaishi nao vizuri na wala hakuna neno na ameshapewa baraka zote amsaidie baba yao.

Halima amesema suala la ndoa yake kufungwa siku ya alhamisi bado ni mapema sana kusema kwani kipindi hiki ni cha kwaresma hivyo muda ukifika watasema jambo lao ni lini lakini kwa sasa hayupo tayari kusema mambo mengi isitoshe yeye sio mwanasiasa .

Mmoja wa watoto wa mzee Mrema ambaye jina limehifadhiwa amesema kuwa , hawana mgogoro wowote na baba yao kuhusu kuoa kwani mzee Mrema ni mtu mwenye akili timamu na anafanya maamuzi yake vizuri na kama wangeona hayuko sawa wangemshauri kwamba sio jambo jema lakini kuhusu suala la baba yao kufunga ndoa kwa kuoa mwanamke familia imelibariki kwani ni mzee na anahitaji uangalizi wa karibu zaidi.

Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates