BREAKING NEWS

Wednesday, March 2, 2022

WATAKIWA KUPANDA MITI ATA MMOJA KATIKA KIPINDI CHA MVUA ILI KUKABILIANA NA TATIZO LA MABADILIKO YA TABIA NCHI

 


 afisa mazingira  kutoka taasisi ya  Lions Clubs International Tanzania Evah  Benson  akipanda mti katika viwanja vya  kikosi cha kutuliza  ghasia mkoa wa Arusha (FFU)  wakati taasisi hiyo ilipopeleka jumla ya miti 300 kwa ajili ya kupanda katika mazingira yanayozunguka kikosi hicho ,afisa huyo alisema  wanampango wa kupanda miti elfu 10000 katika mkoa wa Arusha
afisa kutoka Taasisi  ya  Lions Clubs International Tanzania kanda ya tanzania 411 c,  Masonya Kabwena wa kwanza kushoto  ,kulia ni mkuu wa kikosi cha kutuliza  ghasia mkoa wa Arusha (FFU) Mekidadi Galilima katikati ni afisa mazingira  kutoka taasisi ya  Lions Clubs International Tanzania Evah  Benson wakipanda miti kwa pamoja akipanda mti katika viwanja vya  kikosi cha kutuliza  ghasia mkoa wa Arusha (FFU)  wakati taasisi hiyo ilipopeleka jumla ya miti 300 kwa ajili ya kupanda katika mazingira yanayozunguka kikosi hicho ,afisa huyo alisema  wanampango wa kupanda miti elfu 10000 katika mkoa wa Arusha


Na Woinde Shizza,Arusha  

Ili kuweza kukabiliana na tatizo la mabadiliko ya tabia nchi wananchi wametakiwa kujijengea tabia ya  kupanda miti angala mmoja katika kipindi cha msimu wa mvua  ili  kuweza kubadilisha Tanzania yetu pamoja na kukabiliana na tatizo la mabadiliko ya tabia nchi

 

Hayo yameelezwa na afisa kutoka Taasisi  ya  Lions Clubs International Tanzania kanda ya tanzania 411 c,  Masonya Kabwena alipokuwa akiongea na waandishiwa habari wakati walipokwenda kupanda miti  katika kambi ya FFU Arusha ambapo alisema lengo la kuja kupanda miti ni pamoja na kuhamasisha utunzaji wa mazingira

 

Alisema kuwa taaasi yao imejipanga kupanda jumla ya miti zaidi ya laki moja kwa nchi nzima ya  katika kipindi cha mwaka mmoja lengo likiwa  ni kutunza mazingira  ,kupata matunda  kutengeneza makazi ya viumbe vingine  kama  wadudu na ndege pamoja na kupendezesha nchi yetu

 

Alisema kuwa katika kuanza kupanda miti wameanza na kupanda miti 300 katika kambi ya FFU  Arusha ambapo baada ya hapo wataenda  kupanda miti mingine katika kambi ya FFU NJiro pamoja na taasisi nyingine na kwa mkoa wa Arusha wanampango wa kupanda  jumla ya miti elfu 10000.

 

Kwa upande wake afisa mazingira  kutoka taasisi ya  Lions Clubs International Tanzania Evah  Benson alisema kuwa wanampango wa kupanda miti elfu 10000 katika mkoa wa Arusha  na wataotesha  katika taaasisi mbalimbali zikiwemo mashule ,hospitali na katika sehemu za wazi , huku akibainisha kuwa mbali na hivyo  kupanda miti pia  wanawahimiza wananchi kupanda miti kwani miti ni uhai na pia miti inafanya Tanzania inakuwa ya kijani

 

Akiongea mara baada ya kupokea na  kupanda miti hiyo mkuu wa kikosi cha kutuliza  ghasia mkoa wa Arusha (FFU) Mekidadi Galilima  aliishukuru taasisi hiyo kwakutoa miti hiyo  na kubainisha kuwa wataitunza na kuhakikisha miti hiyo inakuwa  na kufika pale ambapo imekusudiwa  kwani tunapotunza mazingira na nyenyewe yanatutunza

 

 

 

Alisema kuwa wanashukuru kwa namna ambayo wamewatia nguvu na kuwawezesha wameweza kupata miti ambayo itakuwa ni faidi kubwa kwao na hata kwa kizazi kijacho   ambapo pia aliwahakikishia kwa sababu  taasisi  yao ni nyeti na  kubwa   wanaouwezo mkubwa kuhakikisha kwamba miti hiyo wataitunza  kama vile walivyowaamini na kuwaletea maana  hata katika masomo  yao wanayofundishwa wanavyokuwa katika masomo yao wamekuwa wakifundishwa maswala ya  kutunza mazingira .

Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates