BREAKING NEWS

Tuesday, March 22, 2022

TEMDO KUHAKIKISHA TANZANIA INAJITEGEMEA KIVIWANDA




 

mkurugenzi mkuu wa taasisi hiyo Mhandisi Profesa Fredrick Kahimba akiongea na waandishi wa habari walipokuwa katika ziara ya mafunzo ya kuandika habari za sayansi na teknnolojia yalioandaliwa na Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Sayansi Teknolojia na Ubunifu (COSTECH)

Na Woinde Shizza , ARUSHA

 

Taasisi ya Uhandisi na Usanifu wa Mitambo Tanzania (TEMDO) imetekeleza Azimio la nchi kutokuwa tegemezi kwa kutegemea nchi nyingine kwa kuhakikisha kuwa Tanzania inajitegemea kiviwanda kwa kutengeneza teknolojia mbalimbali zinazosaidia kupunguza utegemezi.

 

 Hayo yameelezwa na mkurugenzi mkuu wa taasisi hiyo Mhandisi Profesa Fredrick Kahimba wakati akiongea na waandishi wa habari walipokuwa katika ziara ya mafunzo ya kuandika habari za sayansi na teknnolojia yalioandaliwa na Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Sayansi Teknolojia na Ubunifu (COSTECH) yaliyofanyika kwa muda wa siku tatu katika ukumbi wa mkuu wa mkoa wa Arusha na kufuatiwa na ziara ya siku mbili ya kutembelea taasisi zinazojishulisha na kazi za sayansi na teknolojia ambapo moja ya taasisi waliotembelea ni hiyo

 

Alisema kuwa wameijenga hiyo dhana na kusaidia kupunguza utegemezi wa uagizaji wa bidhaa nje ya nchi bidhaa ambazo zinaweza kutengenezewa na watanzania wenyewe hivyo wameweza kubuni na kutengeneza vifaa tiba hivyo kwani kwa muda mrefu serikali imekuwa ikiagiza vifaa hivyo kutoka nje ya nchi.

 

 


“Kwa mfano katika sekta ya Afya serikali ilikuwa  inaagiza vifaa tiba nje kwa  asilimia 90 na vinavyotengenezwa hapa nchini ni asilimia 10,  sisi TEMDO tuliliona hilo na sasa tunatengeneza vifaa tiba ili kuhakikisha kwamba tunapunguza matumizi mengi ya fedha za kigeni zisizo na sababu kwa kuagiza vifaa tiba na kuhakikisha Sasa vifaa hivyo vinatengenezwa hapa nchini kwa bei nafuu na vinawafikia walengwa kwa wakati,”Alisema Mhandisi Profesa Kahimba.

 

Alisema kuwa  vituo vya afya vilivyojengwa nchi nzima kwa sasa vina  uhakika wa kupata vifaa tiba vyake mkutoka katika taasisi hiyo ya TEMDO badala ya kuagiza tena kutoka nje ya nchi

 

 

 “Tuna teknolojia ya sekta ya kilimo, afya kama nilivyoeleza awali, sekta ya uvuvi, na zaidi sekta ya viwanda vikubwa na  vidogopia tunatengeneza mashine mbalimbali ikiwemo ya kukamulia Alizeti na nifafanue tu mashine hii ya kukamulia mafuta ya Alizeti tumepewa fedha na Tume ya Taifa ya Sayansi Teknolojia na Ubunifu (COSTECH)ambapo tumekabidhiwa kiasi cha shilingi millioni 128 kati ya hizo milioni 65 ni kwaajili ya kutengenezea mashine hii ya kukamulia mafuta ghafi ya alizeti  na fedha zinazobaki tunatekelezea miradi mingine”Alifafanua.

 

hii ndio mashine ambayo Tume ya Taifa ya Sayansi Teknolojia na Ubunifu (COSTECH)imetoa fedha kwa ajili ya kuibuni ambapo kiasi cha  shilingi milioni 65 kimetumika kwaajili ya kutengenezea mashine


Moja ya mfanyakazi anaejitolea wakati akisubiri ajira akiendelea kuchomelea kitanda cha hospitali ambacho vinatengenezwa na taasisi ya TEMDO

 

 

Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates