BREAKING NEWS

Friday, March 4, 2022

MBOWE NA WENZAKE WATATU WAACHIWA HURU

 



MAHAKAMA Kuu, Divisheni ya Rushwa na Ujumumu Uchumi, Dar es Salaam imemuachia huru Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu baada ya Mkurugenzi  wa Mashtaka nchini (DPP) kwa kuwasilisha hati ya kutakuwa na nia ya kuendelea na mashtaka dhidi yao.

Mbowe na wenzake, Adam Kasekwa, Halfani Bwire na Mohamed Ling’wenywa waliokuwa makomandoo wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wameachiwa huru leo Machi 4, 2022 na Jaji Joachim Tiganga.

Mapema kesi hiyo iliitwa mahakamani hapo kwa ajili ya washtakiwa kuanza kujitetea lakini Wakili wa Serikali Mwandamizi, Robert Kidando alieeleza mahakama kuwa  DPP amewasilisha hati (Nolle) kuwa hana nia ya kuendelea na mashtaka dhidi ya washtakiwa.

Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates