YA TANZFOOD JIJINI ARUSHA
Mkurugenzi mtendaji TAHA Dkt,Jackline Mkindi akionyesha Mgeni rasmi unga wa ndizi unaotengenezwa na moja ya kikundi kinachosimamiwa ma taasisi hiyo
Mkuu wa Mkoa wa Arusha John Mongella amezindua maonyesho ya kimataifa ya kilimo TANZFOOD EXPO huku zaidi ya makampuni 120 kutoka Tanzania na nchi jirani zikishiriki
Maonesho hayo yameandaliwa na kampuni ya KILIFAIR Promotion na kuzinduliwa jana tarehe 11/3/2022 katika viwanja vya magereza vilivyopo jijini Arusha
Baada ya kutembea mabanda mbalimbali yaliyoshiriki,Mkuu wa Mkoa Arusha John Mongella alisema maonyesho hayo ni ya siku tatu katika viwanja hivyo na lengo kubwa ni kuleta tija katika mnyororo mzima wa thamani katika kilimo,ufugaji,uvuvi pamoja na uchakataji
Mongella alisema kuwa kupitia maonyesho hayo wadau wa kilimo watapata fursa za elimu katika kujifunza na biashara huku serikali ya mkoa ikipania kufanya kimataifa
Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa TAHA Dkt,Jackline Mkindi ambaye pia ni mwenyekiti wa baraza la kilimo Tanzania alisema kwa sasa sekta ya kilimo imefunguka na ndio inashikilia uchumi wa Taifa
"Masoko yamefunguka sana bidhaa za Tanzania zinagombaniwa kwenye masoko ya kimataifa "alisema Dkt Mkindi
Pia aliongeza kuwa Tanzania ni nchi yenye fursa ya kilimo ukizingatia imezungukwa na nchi nyingi barani Afrika ambazo zinahitaji bidhaa kutoka Tanzania
"Uwepo wa taarifa muhimu za wazalishaji ziliwezesha TAHA kushiriki katika mikutano mikubwa ya kimataifa kama Dubai,Ufaransa pamoja na ubelgiji kuangalia fursa za masoko"alisema Dkt Mkindi
Mkurugenzi wa KILIFAIR Promotion,Dominic Shoo alisema kuwa maonyesho hayo ni fursa kwa wananchi kuweza kujifunza mbinu mbalimbali za kufanya biashara pamoja na kubadilishana mawazo na fursa zilizopo