Na Woinde Shizza,Arusha
Serikali imeobwa kuwekeza nguvu katika kilimo cha la parachichi kwani soko la zao hilo ni kubwa ndani ya nchi na nje ya nchi pia litasaidia kupunguza tatizo la uhaba wa mafuta unaopelekea bei kupanda.
Hayo yameelezwa na Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya AVOMERU GROUP inayojihusisha na mafunzo na ubunifu ya kuchataka bidhaa za maparachichi Jesse Oljange alipokuwa akiongea na waandishi wa habari walipokuwa katika ziara ya mafunzo ya kuandika habari za sayansi na teknnolojia yalioandaliwa na Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Sayansi Teknolojia na Ubunifu (COSTECH) yaliyofanyika kwa muda wa siku tatu katika ukumbi wa mkuu wa mkoa wa Arusha na kufuatiwa na ziara ya siku mbili ya kutembelea taasisi zinazojishulisha na kazi za sayansi na teknolojia
Alibainisha kuwa tatizo la kupanda kwa bei ya mafuta nchini limekuwa kubwa kwani kila siku bei ya mafuta imekuwa ikipanda zaidi hivyo katika kuangalia namna ya kupunguza tatizo hilo kama sio kuondoa kabisa ni vyema Serikali kuamua kuwekeza kwenye viwanda vidogo vinavyozalisha mafuta ya parachichi ili kufanya mafuta hayo kutumika kwaajili ya chakula
“mbali ya chakula pia zao hili la parachichi linaitajika kwa kiasi kikubwa nje ya nchi kwani mbali na kutumika kwa ajili ya chakula pia zao hili mafuta yake yanatujika kwa matumizi mbalimbali kama kutengenezea mafuta ya nywele,mafuta ya ngozi na pia tunda lake hutumik a kwa ajili ya kutengenezea vyakula mbalimbali”alisema Jesse
Alieleza kuwa
zao hilo linafursa nyingi ikiwemo kutunza mazingira, ni tunda, pia mbali na
kukamuliwa mafuta pia kokwa lake kutengenezewa bidhaa za kutunza ngozi hivyo
ifike mahali wakulima wawekeze katika zao hilo ka wingi kwani linachangia
katika ukuaji wa uchumi.
Aidha alisema kuwa uwepo wa kampuni hiyo tangu kuanzishwa
umesaidia wakulima wa zao hilo la
parachichi kuongeza vipato vyao na
kuweza kuendesha maisha yao na sio mkulima tu bali imesaidia kukuzapato la
taifa na kuingizia fedha za kigeni pale wanapoenda kuuza mafuta hayo nje ya
nchi
baadhi ya waandishi wa habari wakifatilia maelezo kutoka kwa
Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya AVOMERU GROUP inayojihusisha na mafunzo na ubunifu ya kuchataka bidhaa za maparachichi Jesse Oljange walipotembelea ofisini kwake
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia