CHID BENZ APATA DHAMANA!

Hatimaye Rapa Rashidi Makwiro, maarufu Chid Benz,leo amefanikiwa kupata dhamana na kutolewa rumande na kurejea uraiani. Anatakiwa kufika mahakamani Novemba 11 ambapo kesi yake itatajwa tena.

Chid Benz 'King Kong' kutoka kundi la La familia Ilala, mchana wa October 28 alisimamishwa kizimbani katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu na kusomewa mashtaka yanayomkabili.
Mashtaka matatu yanayomkabili Chid Benz ni;-
  1. Kukutwa na madawa na vifaa vya kutayarishaji uvutaji wa madawa
  2.  Kusafirisha madawa ya kulevya
  3.  Utumiaji wa madawa ya kulevya
Baada ya kusomewa mashitaka hayo alitakiwa kurudi rumande huku dhamana yake takiwa ikiwekwa wazi kwa masharti ya kuwa na wadhamini wawili wanaotambulika na jumla ya pesa taslim million 1.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia