Ticker

6/recent/ticker-posts

DOLA ZA KIMAREKANI MILIONI MOJA ZATOLEWA KWA WAJASIRIAMALI KWAAJILI YA KUNUNUA MASHINE ZA KUTENGENEZEA BIDHAA MBALIMBALI

Jumla ya kiasi cha  $ 1 milioni sawa na sh,1.6 bilioni kimetolewa kwa wajasiriamali mbalimbali hapa nchini kwa lengo la kuwapatia mashine mbalimbali za kutengeneza bidhaa kama mkopo wa masharti nafuu ili waweze kujikwamua katika biashara zao mbalimbali.
 
Kiasi hicho cha fedha kimetolewa na shirika lililojikita kuwakopesha wajasiriamali wadogo wadogo mashine hizo la Equity For Tanzania(EFTA) katika mikoa ya Arusha,Mwanza,Kilimanjaro,Geita,Shinyanga,Simiyu,Mara na Manyara katika kipindi cha mwaka 2004 hadi 2014.
 
Akizungumza na wakati akifunga Maonyesho ya wajasiriamali waliowezeshwa na EFTA mkuu wa chuo cha Ufundi Arusha DktarIRichard Massika alisema kuwa dhana ya kuwakopesha wajasiriamali mikopo ya Mashine ni dhana nzuri kuliko kutoa pesa ambazo mara nyingi huelekea kwenye shughuli zingine ambazo hazikuwa kwenye lengo lililokusudiwa.
 
Dkta Masika akwataka wajasiriamali waliokopeshwa kuwa mabalozi wazuri wa marejesho ya mikopo ili shirika hilo liweze kutoa mikopo kwa wajasiriamali wengi Zaidi na kujikuta watanzania tunapunguza wimbi la vijana kukosa ajira.
 
“Tufike mahali tukawa wazalendo wa kuwa mabalozi wazuri wa marejesho ya mikopo ili nkuweza kupunguza wimbi la vijana kukosa ajira na shirika lenu lifike mbali Zaidi kwani kuna vijana wenye nia ya kupata nafasi za mikopo ya mashine na teyari wameshaanza shughuli hivyo mufikie hata hao kokote hapa nchini”alisema dkta Masika.

Alisema kuwa watanzania wengi bado wanauhitaji wa kupata mikopo ya kijiinua kiuchumi bila ya kuwaangalia hawa itafika mahali watakosa sehemu ya kuweza kjiinua hivyo kukosa fursa endelevu ambazo zitaweza kuwajengea kipato chao na kukuza uchumi wa taifa.
 
 Awali akimkaribisha mgeni rasmi kabla ya kufunga Maonyesho ya bidhaa zinazotengezwa na shirika hilo,meneja masoko wa shirika hilo,Peter Temu alisema kuwa mikopo hiyo yenye masharti nafuu imetolewa kwa lengo la kuwakwamua wajasiriamali hao ili waweze kupiga hatua katika biashara zao.
 
Temu,alisema kuwa changamoto kuu ambayo wamekuwa wakikumbana nayo katika majukumu yao ni pamoja na baadhi ya wateja wao kutorudisha mikopo hiyo kwa wakati hali ambayo imekuwa ikiwakwanza katika kutekeleza majukumu yao.
 
Awali meneja wa oparesheni na mipango wa shirika hilo,Tim Ellis alisema kuwa mkakati wao hapo baadaye ni kupanua huduma yao katika mikoa minane zaidi na kuwafikia watanzania wengi hususani walio katika maeneo ya vijijini .
 
Alisema kwamba wamekuwa wakishirikiana na wafadhili mbalimbali katika majukumu yao huku akiwataja baadhi yao kuwa ni pamoja na benki ya dunia(WB),Africa Enterprise Challenge Fund(AECF) pamoja na wawekezaji binafsi walioko hapa nchini.

Post a Comment

0 Comments