Ticker

6/recent/ticker-posts

KINANA AMALIZA ZIARA YAKE JIMBO LA MTAMA


01
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na Bernard Membe Mbunge wa jimbo la Mtama na Mjumbe wa Halmashauri kuu ya taifa wakati alipowasili katika Kiwalala Kituo cha Ufugaji cha Masister cha Narunyu ambapo ameshiriki kazi ya kukamua maziwa akiwa katika ziara yake ya kikazi ya mikoa ya Lindi na Mtwara akikagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 inayotekelezwa na serikali lakini pia kuhimiza uhai wa Chama cha Mapinduzi CCM, Katibu mkuu Kinana katika ziara hiyo anaongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa,Itikadi na Uenezi.
3
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kazi ya kukamua maziwa katika kituo cha uugaji cha Masister cha Narunyu Mtama mkoani Lindi wakati alipotembelea kituo hicho.02
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na baadhi ya Masister mara baada ya kuwasili katika kituo hicho katika jimbo la Mtama mkoani Lindi.1
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akionyesha kitabu kinachoelezea shughuli mbalimbali zilizotekelezwa na Mbunge wa jimbo la Mtama Mh. Bernard Membe alipotembelea ofisi ya mbunge huyo. 11
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki katika shughuli za kubangua korosho wakati alipotembelea kikundi cha akina mama cha kubangua korosho katika kata ya Nyegendi jimbo la Mtama.

Post a Comment

0 Comments