Ticker

6/recent/ticker-posts

WAPENDA AMANI NCHINI WALAANI TAMKO LA JUKWAA LA WAHARIRI.


Na Sheila Simba-Dar es salaam.

Wapenda amani nchini wamelaani kitendo cha Jukwaa la Wahariri (TEF)kutoa tamko dhidi Serikali kuhusu kufungia vituo viwili vya redio hivi karibuni.

Wakiongea kwa nyakati tofauti Jijini Dar es Salaam, wameonyesha Dhahiri kuchukizwa na TEF na kusema hawajui wanalolifanya.

Bwana Juma Ramadhan, Mkazi wa Ilala, amesema kuwa hapendezwi na watu kutetea chombo kinachohatarisha amani Nchi na mali zao kwa kuandika habari za uchochezi.
“Mimi nimekaa nchini kwa kipindi kirefu sijaona machafuko je huyu anayechochea uvunjifu wa amani ana lengo gani kwa Taifa?”, aliuliza Ramadhani

Naye  Bi Mercy Mwakitalima Mkazi wa Sinza, amesema kuwa Jukwaa hilo linapaswa kusimamia na kuongoza vyombo wanavyosimamia kutokutumia maneno na lugha isiyofaa ili kuepeka kuliingiza taifa katika machafuko.

Ameongeza kuwa wahariri wanapaswa kusimamia maadili ya uandishi wa habari ili vyombo vyao viandike habari zinazingatia umoja kitaifa uliojengeka kwa muda mrefu.

“Taifa letu ni la amani na inatakiwa kulindwa kwa gharama yoyote,naviomba vyombo vya habari nchini kuheshimu sheria za Nchi,ki ukweli siku hizi baadhi ya vyombo wanaongea sana vitu ambavyo havina faida yoyote kwa jamii, naipongeza Serikali kwa hatua waliochukua ili iwe fundisho kwa wengine”alisema Mwakitalima

Ameongeza kuwa sekta ya habari nchini inatakiwa kuwa mstari wa mbele katika kuhubiri amani na sio kutumia maneno yanayochochea uvunjifu wa amani kwani kufanya hivyo kutapelekea Taifa pabaya kwa kuwalisha watanzania vitu visivyofaa.

Kwa upande Mwalimu wa shule ya Msingi Kinondoni aliyejitambulisha kwa jina moja la Mwamvua,ameiomba Serikali kuharakisha Muswada habari ili kuwa na watu wenye sifa pekee katika sekta ya habari kwani kwasasa sekta ya habari imepoteza umaarufu wake.

“sekta ya habari nchini kwa sasa haina mwelekeo kila mtu ni mwandishi wa habari bila hata kuwa na taaluma ya habari hili ni tatizo lazima Serikali ilifanyie kazi mapema ili kuepeuka kuwa na watu wasiojua maadili ya kazi hiyo,”alisema Mwamvua.

Naye Joseph Jeremia ameomba Serikali kuendelea kuvichukulia hatua vyombo vya habari ambavyo vinamwelekeo wa kuhatarisha amani ya Tanzania kwa kuvifuta kabisa.

Amesema amani ni rahisi kuipoteza lakini ni kazi ngumu kuijenga kama ilivyo hapa nchini.

Jukwaa la wahariri walitoa tamko hilo, kufutia Serikali kupitia kwa Waziri wa Habari,Sanaa,Utamaduni na Michezo Nape Nnauye, kutangaza kufungia vituo viwili vya radio kwa kutangaza habari za uchochezi,ambazo ni Radio five ya Arusha na Radio Magic fm ya jijini Dar es salaam.



Post a Comment

0 Comments