Ticker

6/recent/ticker-posts

JESHI LA CHINA LAELEKEA KUWEKA KAMBI YA KWANZA YA KIGENI DJIBOUTI



Meli zinazowasafirisha wanajeshi wa China zinaelekea nchini Djibouti kuweka kambi ya jeshi ya China ambayo ndiyo ya kwanza ya kigeni.

China inasema kuwa kambi hiyo itatumiwa kwa huduma za kulida amani na za kibinadamu barani Afrika na magharibi mwa Asia.

Pia itatumiwa kwa ushikiano wa kijeshi, mazoezi ya kijeshi na huduma za uokoaji.
China imewekezaa katika nchi za kiafrika na pia imeboresha kwa haraka jeshi lake miaka ya hivi karibuni.
Shirika la habari ya Xinhua lilisema kuwa meli hizo ziliondoka bandari ya Zhanjiang katika mkoa wa kusini wa Guangdong siku ya Jumanne.
Halikutaja idadi ya wanajeshi au meli zilizoplelekwa Djibouti au ni lini kituo hicho kitaanza kutangaza huduma zake.
Xinhua linasema kuwa kituoa hicho cha Djibouti kinabuniwa kufuatia mazungumzo kati ya nchi hizo mbili.
Kituo hicho kinaonekana kama hatua ya China ya kuwa na usemi wa kijeshi eneo hilo.

Trump ashtakiwa kwa kuwazuia wakosoaji katika Twitter


Rais wa Marekani Donald Trump kwa muda wa miaka 30 amekabiliwa na zaidi ya na kesi 4,000
Na sasa mwanabiashara huyo ambaye sasa ni Rais, ameshtakiwa kwa mara nyingine, baada ya watu saba kumshtaki kwa kuwazuia kwenye akaunti yake ya twitter.

Bwana Trump ni mtumiaji mkubwa wa mitandao ya kijami ambayo anaituma kuwapongeza washirika na kuwashambulia mahasimu wake.
Kesi hiyo iliwasilishwa mahakamani na taasi ya Knight First Amendment Institute, ambalo ni kundi la kupigania uhuru wa kusema katika chuo cha Columbia.
Watumiaji hao saba walisema kuwa akaunti zao zilifungwa na rais au wasaidizi wake, baada ya wao kukejeli au kukosoa ujumbe alioandika Trump.
Watumiaji wa Twitter hawan uwezo wa kuona au kujibu ujumbe katika akaunti zinazowazuia.
Mashtaka hayo ni kuwa kwa kuwazuia watu hawa, Bwana Trump amewazuia kujiunga na majadiliano ya mtandaoni.

Post a Comment

0 Comments