Ticker

6/recent/ticker-posts

MFUMUKO WA BEI WA TAIFA KWA MWEZI JUNI,2017 WAPUNGUA KWA ASIMILIA 5.4

 Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Ephraim Kwesigwabo (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leokuhusu mfumuko wa bei wa Taifa kwa Mwezi Juni. Kulia  ni Meneja wa Takwimu za Bei na Ajira, Ruth Minja.
 Mkutano na wanahabari ukiendelea.
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.

Na Dotto Mwaibale

MFUMUKO wa bei wa Taifa kwa mwezi Juni  umepungua hadi kufikia asilimia 5.4 ikilinganishwa na asilimia 6.1 ilivyokuwa mwezi Mei 2017.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Sensa na wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari Dar es Salaam leo mchana kuhusu mfumuko huo wa bei.

Kwasigabo alisema kasi hali hiyo inamaanisha kuwa kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2017 imepungua zaidi ikilinganishwa na kasi iliyokuwa kwa mwaka ulioishia mwezi Juni, 2017.

"Fahirisi za bei zimeongezeka hadi 109.10 mwezi Juni,2017 kutoka 103.47 mwezi Juni 2016" alisema Kwesigabo.

Alisema mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwezi Juni 2017 umepungua hadi hadi asilimia 9.6 kutoka asilimia 11.6 ilivyokuwa mwezi Mei,2017

Alisema mfumuko wa bei kwa kipimo cha mwaka kwa bidhaa za vyakula nyumbani na migahawani kwa mwezi Juni 2017 umepungua hadi kufikia asilimia 9.8 kutoka asilimia 11.8 mwezi Mei 2017.

Aliongeza kuwa badiliko la fahirisi za bei kwa bidhaa zisizo za vyakula umeongezeka hadi asilimia 3.11 mwezi Juni 2017 kutoka asilimia 3.1 mwezi Juni, 2017 kutoka asilimia 3.0 mwezi Mei 2017.

Post a Comment

0 Comments