Ticker

6/recent/ticker-posts

NABII MKUU MH DK. GEORDAVIE: NAWAOMBA WANANGU MUWE NA MOYO WA KUSAMEHE.


Nabii mkuu Tz Mh Dk. GeorDavie amewataka watu kuwa na moyo wa kusamehe pale wanapokoseana ikiwa ni pamoja na kuwa na umoja ili waweze kusimama imara katika maeneo mbalimbali maishani.
Nabii Mkuu Tz Mh Dk. GeorDavie ameyasema hayo jana katika ibada ya jiji iliyofanyika katika hema la kukutania chuo kikuu cha manabii kisongo Arusha ambapo ilikuwa siku ya Jumapili ya kusanyiko
Pia katika mafundisho yake Nabii Mkuu Mh Dk. GeorDavie amewataka watu popote wanapokwenda wasiache kuikumbuka nguvu ya mungu iliyowainua kwani nguvu hiyo ndio imekuwa nguzo katika maisha yao yote.
Aidha, Nabii Mkuu Mh Dk. Geordavie pamoja na mchungaji kiongozi Mama Anna Davie wanatarajiwa kuwepo radioni leo majira ya saa mbili na nusu hadi saa tatu na nusu  usiku katika kipindi cha kusapoti magurudumu ya radio.  
Pia katika kipindi hicho Mh. Nabii Mkuu atafafanua kuhusu ujio wake wa Jumapili hemani kisongo, Ratiba ya Pipa day pamoja na kutamka matamko ya kinabii.

Post a Comment

0 Comments