Ticker

6/recent/ticker-posts

UVCCM:LISSU AMECHOKA MAISHA YA URAIANI



Na Mwandishi Wetu, Kigoma

Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) umesema matamshi  yaliotamkwa na Mbunge wa Singida Mashariki(Chadema)Tundu Lisu ni ya kusaka umaarufu wa kisiasa hatimae   awanie  urais akiwawacha solemba  Edward Lowassa na mshirika wake Fredrick Sumaye .

Aidha Umoja huo umesema povu linalowatoka viongozi wa upinzani akiwemo Lisu, ni kielelezo cha kutapatatapa na kufiisika kisiasa kufuatia utendaji unaokubalika wa serikali   ya Rais john Magufuli huku wakiwa wakionekana kuvunjika matumaini na kukata tamaa. 

Hayo yametamkwa jana na Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM  Shaka Hamdu Shaka wakati alipozumguza na viongozi, wanavyuo na wanachama wa CCM katika ukumbi wa CCM  kizota mjini kigoma mkoani hapa. 

Shaka alisema maneno ya Lisu hayawezi kuitingisha serikali ya CCM  na kwamba serikali inayomnanga iwapo  itamtaka akamatwe kwa kuvunja sheria za nchi, vyombo vya  dola havitasita kumuweka kizuizini .

Alisema kuna kila ishara ya mwanasiasa huyo wa upinzani inayoonyesha akiyatamani maisha ya gerezani  baada ya kuchoshwa na yale ya uraiani ambapo sasa ameamua kutamka upuuzi , kujeli na upumbavu kinyume na ustaarabu.

"Tumemtafakari na kubaini ana nia ya kuwania urais mwaka 2020, anachotaka ni kuwaacha kwenye mataa jamaa zake kina Lowasa na sumaye, ila ajue akizidi kueneza matamshi ya kipuuzi anaweza kukamatwa na kutupwa mahali"Alieleza shaka 

Alisema hakutawakuwa hakuna maana ikiwa mtu mmoja anainanga Serilali na kuipaka matope, kumkejeli Rais akiyewekea kisheria na kikatiba na wananchi wkaendelea kutazamwa macho. 

"Lisu si kama papai ambalo kama litaweka ndani litaooza na kuharibika, anaweza kukaa huko kwa usalama wake na wa nchi,tuneruhusiwa kisheria kufanya siasa za vyama vingi kwa ustaarabu na uungwana na si kufanyiana kejeli na dhihaka "Alieleza 

Alisema hata wakati wabutawala wa Baba wa Taiafa mwalimunjulius nyerere walikywepo baadhi ya wanasiasa waliotaka kuidharau serikali,walikamatwa kwa usalama wao na kufichwa mahali kwa muda fulani. 

"Lisu ni nani mbele ya mamlaka za kisheria na kikatiba, tunadhani anatatapata nyingi nasaba hivyo ajiandae siku yoyote anaweza kukutwa na msiba,msiba wa kujitakia hauna pole, dola yoyote haifanani na kitambaa cha deki" Alisisitiza. 

Uvccm ina ushahidi wa kutosha toka kwa watu wa karibu na Lisu wamemwambia kwamba ndiye snayetosha kuwania urais ndani ya chadema mwaka 2020 hivyo ametakiwa atafute "kick'ya kisiasa ili kuvuruga Sumaye na Lowassa .

Hata hivyo shaka alisema si kosa kwa Lisu kuwania urais ila anachotakiwa ni kujipima kibusara na kibusara, kiuwezo na kiupeo kama ni mtu anayestahili na sahihi ambaye  anayetosha kuomba nafasi hiyo au la  .

Vile vile uvccm umewataka watanzania kumpuuza mwanasiasa huyo wa chadema kwa kadri atakavyotamka kwasababu mtu yoyote mwenye ufahamu na uelewa hawezi kuyadhijaki mamlaka ya Rais na nafasi alionayo. 

"Ujasiri wa kuidhihaki mamlaka ya Rais ni sawa na mtu juha aubounguani anayejaribu kutupa jiwe katikati ya mzinga wa nyuki au mpumbavu kuncgeea simba sharubu "Alieleza shaka. 


Kaimu huyo katibu mkuu aliwashukuru wazee wa mkoa wa kigoma kwa kumtawaza na kuwa mwana kigoma huku akiwaahii hatawangusha ila malipo anayoyaanda kuonyesha shukran na furaha yake ni kuongiza harakati za kisiasa zitakazomuondoa zito Kabwe kwenye nafasi ya ubunge wa kigoma mjini mwaka 2020 . 

Post a Comment

0 Comments