Ticker

6/recent/ticker-posts

ZITTO AMEVUNJA MKATABA MUHIMU KIGOMA :UVCCM





Na Mwandishi Wetu, Kigoma

Umoja wa Vijana wa CCM umesema siku za uwakilishi za Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe zinahesabika kwani wananchi watampata somo maalum ifikapo mwaka 2020 kwasababu ameshavunja mkataba kati yake na wananchi waliompatia dhamana ya kuwatumikia hivyo toka sasa atazamwena tu kupuuzwa.

Aidha Umoja huo umesisitiza kwasababu mbunge huyo ana historia na kujifanya  kujua kwingi, kutoshaurika na kutopenda ushirkiano na wenzake kuna kila ishara zinazoonyeaha atasombwa na mvua ya kisiasa na kutupwa kwenye maporomoko ya Ziwa Tanganyika.

Matamshi hayo yametamkwa jana  na Kaimu Katibu Mkuu Shaka Hamdu Shaka alipokuwa akizungumza na viongozi wa Matawi, Kata na wilaya na wanachama wa CCM  na jumuiya zake katika kata ya Gungu wilaya ya Kigoma Mjini  .

Shaka alisema mwanasiasa huyo ana historia ya hovyo ya kutofahamiana na wanasiasa wenzake toka akiwa chuo kikuu Dar es salam , alipojiunga Chadema akafukuzwa na sasa hawivi na wenzake huko  ACT Wazakendo.

Alisema kulikuwa hakuna sababu hata moja ACT Wazalendo chini ya uongozi wa Zitto kupitisha maamuzi ya kumvua wadhifa aliyekuwa Mwenyekiti wake Anna Mghwira kwasababu tu ya kuteuliwa na Rais Dk John Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro .

"Siku zake mtu huyu za kubaki katika uga wa siasa zimegota , hatabaki katika uso wa siasa , naamini atasombwa na mawimbi ya Ziwa Tanganyika na kufutika kurasa za siasa, haambiliki, mbabe na hapendi maelewano na wenzake, mwaka 2020 atakiona cha mtema kuni "Alisema Shaka. 

Alisema kiongozi huyo Mkuu wa ACT Wazalendo ni mtu asiyefahamika kwakuwa leo anaweza kusema jambo hili ukamuona kama mzalendo halisi laikini kesho akageuka na kusema mambo yanayoonyesha ni mwanasiasa mtata na mtatanishi .

"Nawaomba sana wananchi wa kigoma endeleeni kuiunga mkono ccm na ssrikaki yake katika kuendeleza amani, maendeleo, umoja na mshikamano, acheni kughiibiwa na kughilibika kwa mambo ya kupita , chama chenu  ni ccm hivyo vingine ni kampuni binafsi za vigogo wa vyama hivyo 'Alisema 

Shaka aliwataja wanasiasa wakongwe akiwemo aliyekuwa Waziri  katika Serikali ya kwanza ya Tanganyika huru Marehemu Sheikh Amri Abeid Karuta na mmoja kati ya waasisi 17 wa chama cha TANU hayati Mzee Saadan Abdul Kandoro na wanasiasa wengine walisaidia sana katika kupigania Uhuru  pia wapo walioshiriki na kufanikisha Mapinduzi matukufu  ya Zanzibar. 

Vike vike shaka aliwataka wanachama wa CCM  kujichuja, kuwabaini na kisha kuwatimua wanachama wasaliti wenye ndimi mbili ambao mchana huvaa sare za ccm na kuiba mikakati na siri za chama lakini  usiku watu hao hubadilika na kujivika magwanda .

"Mwanachama atakayebainika kwa ushahidi kamili ameshiriki kutenda usaliti atimuliwe , Chama Cha Mapinduzi hakina tena njaa ya wanachama hivyo mtu atakayeyumba au kuonyesha unafiki lazima aondoke kama wengine walivyofukuzwa "Alisisitiza Shaka  

Kaimu huyo Katibu Mkuu alisema usaliti ni jambo baya na ovu lisilovumilika kwani kama watu wa aina hiyo wangekuwepo nyakati za kupigania uhuru na kupanga mbinu za kufanikisha mapinduzi, mambo yangekwama hatimaye usultan na ukoloni ungelibaki hadi leo .

Hata hivyo kaimu katibu mkuu huyo alifanya harambee ya papo kwa papo ya kufanikisha ujenzi wa ofisi ya ccm kata ya Gungu ambapo wanachama na viongozi walichangia jumla ya shilingi 355,000 huku mbunge wa vijana Mkoa Kigoma Zainab Katimba akichangia bati mia moja.

Post a Comment

0 Comments