BAADA YA KOCHA BRIAN McDERMOTT KUACHIA NGAZI READING, SASA KOCHA WA KUVAA VIATU VYAKE KUTAFUTWA HARAKA.
McDermott (51) ndiye aliyewaongoza Reading kupanda daraja msimu uliopita, akachaguliwa kuwa kocha bora wa mwezi hivi karibuni, lakini tangu hapo timu yake imepoteza mechi nne mfululizo.
“Mmiliki Owner Anton Zingarevich anamshukuru Brian kwa kazi yake. Utafutaji wa kocha mpya unaanza mara moja, na matarajio ni kujaza nafasi hiyo haraka iwezekanavyo.
Zingarevich ameona ulazima wa kufanya mabadiliko,” taarifa ya klabu inasema.
McDermott alijiunga Reading 2000 akifanya kazi chini ya Alan Pardew ambaye sasa ni kocha wa Newcastle United.
Mwaka 2009 baada Reading kumfukuza kazi kocha wao, Brendan Rodgers (sasa bosi wa Liverpool wanaofanya vizuri), McDermott alipewa ukocha wa muda kabla ya kuwa kocha kamili.
*************************************
UNITED WAMTEGA CR7...
0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia