LOWASA ASAIDIA KUKUSANYA SH 85 MILIONI ZA AJIRA KWA VIJANA WA PIKIPIKI MKOANI ARUSHA



Waziri mkuu aliyejiuzulu Edward Lowassa.  

Waziri mkuu aliyejiuzulu Edward Lowassa amefanikisha kukusanywa kwa Sh85 milioni katika harambee ya kukusanya fedha kwa ajili ya kutatua tatizo la ajira kwa vijana, mkoani Arusha.
Harambee hiyo iliyofanyika juzi, iliandaliwa na Umoja wa Waendesha Pikipiki (Uwapa) wa Jiji la Arusha.
Akizungumza katika harambee hiyo, Lowasa ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, aliwataka vijana kujiepusha na ushawishi wa wanasiasa wanaowarubuni ili kushiriki katika maandamano yasiyokuwa na tija.
Badala yake, aliwataka wajikite katika kuzungumzia maendeleo yao. Alisema fedha zilizopatikana katika tukio hilo, ni vyema zikatumika katika kukopeshana ili kupanua mitaji ya biashara zao.

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

Previous Post Next Post