Ticker

6/recent/ticker-posts

KESI YA SHAMBULIO KWA PANGA MSIKITINI BADO KIZUNGUMKUTI



Na Mwaandishi Wetu,


Jalada la lalamiko katika kesi inayomkabili mtumiwa ambaye ni

mfanyabiashara mwenye asili ya kiasia Abdulrazak Othman Mohamed  (43)
kumshambulia na kumjeruhi kwa panga Katibu wa Msikiti wa Jumuiya ya
Wamakonde uliopo Mtaa wa Nyamwezi na Amani jijiji Dar es Salaam imekwama
kwa Wakili wa Serikali  na haijafkishwa Mahakamani.

Abdulrazak alimshambulia na kumjeruhi Katibu wa Msikiti wa Wamakonde

Abdallah Saiwaad kwa kumpiga mapanga matatu kichwani, begani na mkononi na
kumjeruhi mwilini hadi kulazwa katika hospital ya Taifa ya Muhimbili jijini
Dar es Salaam.

Saiwaad akiwa na wajumbe watano wa kamati ya Msikiti Wamakonde (wiki tatu

nyuma )walifila dukani kwa mpangaji wa dula la Msikiti  Abdulrazak kwa
ajili ya kufuatilia deni la kodi ya pango ambapo mtuhumiwa  alidaiwa
kumshambulia na kumjeruhi Katibu huyo.

Baada ya kumjeruhi kwa panga, alitoweka hadi alipotiwa nguvuni na polisi,

kuchukukiwa maelezo katika kituo cha polisi Msimbazi baadae akapata dhamana
na sasa anaendelea na kazi yake ya kuuza duka katika Mtaa wa Amani na
Nyamwezi maeneo ya jangwani .

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala RPC Salim Rashid ameiambia uhuru kuwa

shitaka hilo limeondoka mikononi mwa polisi na kwamba  liko chini ya
dhamana ya Ofisi ya Wakili wa Serikali kanda ya Dar es salaam hivyo hajui
kinachoendelea.

"Tumekamilisha jukumu letu kama polisi, jalada la kesi  liko ofisini kwa

Wakili wa Serikali Kanda ya Dar es Salaam kwa hatua zaidi, sina uwezo wa
kulizungumzia jambo  hilo kwani haliko tena katika dhamana ya polisi
"Alisema Kamanda  Salim.

Juhudi za kumpata Wakili wa Serikali Kanda ya Dar es salaam zilishindikana

baada ya kutokea ishara za urasimu  katika ofisi yake huku baadhi ya
wahudumu wakionekana  kumkatisha tamaa mwandishi aliyefuatilia shauri hilo
ili kujua hatma ya kesi hiyo.

Baadhi ya waumini katika Msikiti wa wamakonde wameelezea kusikitishwa kwao

na maendeleo ya ukimya wa kesi hiyo huku aliyejeruhi akiendelea na shughuli
zake kama kawaida licha ya kukabiliwa na shitaka la kudhuru kwa kutumia
silaha.

Siraji Mfaume Idd (34)mkaazi wa Mtaa wa Muhoro  alisema kinachoendelea ni

aibu kwa kwa waislam na vyombo vya sheria kuona mtu amepigwa, ameumizwa
kinyume na ubinadamu akikosa utetezi wa haki na aliyedhuru akidunda mitaani.

Alisema kitendi hicho kimewahuzunisha  waumini wa Msikiti wa Wamakonde kwa

kushuhudia haki ikitaka kubakwa na kuwekwa mfukoni bila  ya sababu za
msingi huku Baraza la Waislam Tanzania  (BAKWATA )likiwa kimya bila
viongozi wake kupigania haki ya kiongozii  wa Msikiti .

"Waislam hatuna mtetezi zaidi ya kumtegemea  Allah, angepigwa muumini

mwingine aidha kanisani au kwenye hekalu, haki ingepatikana na hatma ya
uamuzi wake kwa mujibu wa sheria ungefahamika "alieleza Siraj.

Hemed Halfan "Killer" anayeishi Mtaa wa Ndovu alisema kuzorota kwa shauri

hilo na kutosikilizwa huku aliyejeruhi akifanya biashara kama vile
hakutenda kosa katika eneo ambalo ni  miliki ya Msikiti  kwa  kudaiwa kodi
ni udhaifu wa kamati ya Msikiti na viongozi wa BAKWATA Mkoa wa Dar es
salaam .

Hemed alisema itakuwaje Katibu wa Msikiti apigwe , aumizwe na ajeruhiwe na

mpangaji halafu wajumbe wa kamati ya msikiti wakae kimya kama is uzandiki
na kukosa umoja.

"Wajumbe wa kamati nafikiri  wanazunguukana nwenyewebkwa wenyewe ili

kumsaliti katibu wa msikitini, mungu hatakubali hata siku moja haki iwe
batili na batili isimame kama  sheria na ishara ya haki "alieleza Hemed.

Sheikh wa BAKWATA Mkoa wa Dar es salaam Sheikh Alhad Salum  alipotafutwa

ili kuelelezea hatma ya shauri hilo ilielezwa yuko safarini mkoani singida
kuhudhuria maadhimisho ya sherehe za Maulid ya kuzaliwa kwa kiongozi wa
dini ya kiislam duniani  Mtume M.uhammad  ('S. A.W)

Alipotafutwa Mwenyekiti wa Kamati ya Msikiti wa Wamakonde Ustaadh Kitwana

Abdulrahman simu yake ya kiganjani  muda wote iliita bila kupokewa kwa muda
mrefu.

Post a Comment

0 Comments