Ticker

6/recent/ticker-posts

MWANDISHI WA HABARI WA ITV ARUSHA AACHIWA HURU

 Mwandishi wa Habari wa ITV na Redio One Khalfan Liundi (Mwenye shati jeupe)  akitoka katika kituo cha Polisi cha Usariver Mara baada ya kupata dhamana,alikamatwa kufuatia amri ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Alexender Mnyiti kwa kutuhumiwa kuandika habari za uchochezi
 Mwandishi wa Habari wa ITV na Redio One Khalfan Liundi (Mwenye shati jeupe)  akitoka katika kituo cha Polisi cha Usariver Mara baada ya kupata dhamana,alikamatwa kufuatia amri ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Alexender Mnyiti kwa kutuhumiwa kuandika habari za uchochezi

Mwandishi wa Habari wa ITV na Redio One aliyekua ameshikiliwa na jeshi la polisi wilaya ya Arumeru na kuwekwa mahabusu  kwa zaidi ya masaa 24 kwa kile kinachodaiwa  kuwa ni agizo la Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Alexender Mnyiti ameachiliwa kwa dhamana.

Liundi alikamatwa Disemba 21 majira ya saa 8 mchana ambapo awali alifunguliwa shtaka la kuandika habari za uchochezi ,ambalo hata hivyo  katika hali ya sintofahamu leo asubuhi polisi katika kituo cha Usariver walikanusha kwamba hakukuwa nan shitaka lolote isipokua wanafuata agizo la mkuu wa Wilaya la kumuweka mahabusu.

Akizungumza mara baada ya kuachiwa kwa dhamana leo majira ya saa 9:30 alasiri Liundi amesema katika mahojiano na Askari wa upelelezi ametuhumiwa kuandika habari nyingi zinazohusu malalamiko ya wananchi bila kile kinachoelezwa kusikiliza upande wa Uongozi  wa Wilaya.

Mwanasheria wa Mwandishi huyo kutoka Tume ya Haki za Binadamu Edwin Silayo amesema Liundiameachiwa kwa dhamana ya Shilingi milioni 10 na wadhamini wawili huku akitakiwa kuripoti katika kituo hicho cha polisi Disemba 27.

Tukio la kukamatwa kwa Liundi limewagusa  Waandishi wa habari vyombo vya habari vya  kitaifa na kimataifa ambao wameonekana kusimamisha shughuli zao na  kupiga kambi katika kituo hicho kwa siku zote mbili.

Post a Comment

0 Comments