BREAKING NEWS

Friday, July 22, 2022

IGP WAMBURA AWATAKA WANANCHI WA MKOA WA ARUSHA KUENDELEA KULINDA AMANI

 


MKUU wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Camilus Wambura amewataka wananchi wa jiji la Arusha kuendelea kutunza amani iliyopo na kutokujiingiza kwenye vitendo vya uvunjifu wa amani hasa kipindi hiki ambapo kuna mkutano mkubwa wa Maras kutoka nchi saba za afrika mashariki.

IGP Wambura amesema hayo baada ya kupokelewa Makao Makuu ya Polisi mkoa wa Arusha na kupokelewa na kamanda wa Polisi mkoani humo Justin Masejo ambapo aliwataka askari kuendelea kusimamia amani na kuwachukulia hatua kali wale wote watakaobainika kutaka kuvuruga amani ya nchi.

Na kuahidi kushughulika na yeyote ambaye atakuwa na vitendo vyovyote kinyume na maadili na kinyume na matendo mema ya Watanzania.

Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates