BREAKING NEWS

Thursday, July 14, 2022

WADAU WA UTHIBITI WA MAAFA WAKUTANA KUJADILI NA KUDHIBITISHA MPANGO WA TAIFA WA KUJIANDAA NA KUKABILIANA NA MAAFA


 

 W

Jenerali Michael Mumanga Akizungumza na wadau wa maafa jijini Arusha.

 

 
Ofisi ya Waziri Mkuu katika kutekeleza Sheria ya usimamizi wa maafa imeànza kuimarisha uratibu wa shughuli za udhibiti wa maafa kwa kuhakikisha uwepo wa mfumo thabiti katika ngazi Zote

Katika ufunguzi wa jukwaa la Wadau wa udhibiti wa maafa kwa ajili ya kujadili na kudhibitisha mpango wa Taifa wa kujiandaa na kukabiliana na maafa na mkakati wa mawasiliano wakati wa dharura uliowakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya maafa jijini Arusha

Mkurugenzi idara ya menejiment ya maafa kutoka Ofisi ya waziri Mkuu Meja Jenerali Michael Mumanga,anasema lengo la jukwaa hili Ni kutoa fursa kwa Wadau kutoa maoni yao kwa lengo la kuboresha na kuthibitisha mpango ulioandaliwa

Jenerali Mumanga anasema kutokana na kuongezeka kwa matukio ya majanga ambayo yamekuwa yakisababisha maafa,serikali kwa kushirikiana na wadau wameona Ni muhimu kuwa na mipango mikakati yenye lengo la kujiandaa na kupunguza vihatarishi vya maafa

"Mipango hii mikakati ni kuhakikisha kuwa pindi maafa yanapotokea ni namna gani nchi itawajibika katika kutatua au kupunguza maafa hayo" Alisema jenerali

Kwa upande wao Wadau wa maendeleo wanasema kukutana kwa wataalam Hawa Kuna lengo la kupitia na kujadili namna ya kupunguza athari za majanga

Mpango huu wa Taifa wa kujiandaa na kukabiliana na maafa ulianza mwaka 2012 ukizishirikisha Taasisi za kiserikali na zisizo za kiserikali.

Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates