BREAKING NEWS

Tuesday, July 12, 2022

TIMU YA TAIFA YA TAEKWONDO YAONDOKA KWENDA NCHINI RWANDA KUSHIRIKI MASHINDANO YA UBIGWA KUSAKA UBIGWA WA AFRIKA

 


Picha ikionyesha  wachezaji wa timu ya taifa ya Taekwondo  pamoja na kocha wa timu hiyo ya taifa  mwenyewe asili ya kichina walioenda kuwakilisha nchi katika mashindano ya kusaka  ubigwa wa mchezo wa  Taekwondo  Afrika yanayofanyika yanayo tarijiwa kuanza kutimua vumbi July 13 hadi 17 mwaka huu nchini Rwanda (picha na Woinde Shizza)



 

Na Woinde Shizza ARUSHA 


Timu ya taifa ya mchezo wa  Taekwondo  imeondoka leo nchini kueleekea nchini Rwanda kwa ajili ya kushiriki mashindani ya ubigwa wa mchezo huo kwa nchi za afrika yanayoa yanayotarajiwa kuanza July 13 hadi 17 nchini humo.

 Akiongea  na waandishi wa habari mkurugenzi wa ufundi wa shirikisho la Taekwondo Tanzania Richard Kitolo alisema kuwa timu ya taifa ya mchezo huo inatarajiwa kuondoka leo July kwenda nchini Rwanda kwa ajili ya kushiriki mashindani ya kusaka ubigwa wa Afrika wa mchezo huo.


Alisema kuwa katika mashindani hayo nchi 40 kutoka afrika zimethibitisha kushiriki  mashindano hayo yatakayo fanyika  katika uwanja wa Arena Kigali nchini Rwanda,huku akibainisha kuwa jumla ya wachezaji wanne na viongozi wawili  wanatarajiwa kuondoka kwenye msafara huo


Akibainisha kuwa maandalizi yamekamilika na wachezaji wote wapo vizuri  kwa ajili ya kwenda kushiriki mashindano hayo.

Kwa upande wake kocha mkuu wa timu ya taifa ya Taekwondo  Kim Keumloon  alisema maandalizi ya wachezaji yamekamilika  na wamefanya mazoezi yakutosha   na wanaimani watakuja na ushindi 

"Tumefanya mazoezi kwa kadri ya uwezo wetu tunaamini tutashinda na kuleta ushindi nyumbani na kuletea ushindi nchi ,japo tunajua timu kule kuna  Kuna timu zilizofanya mazoezi yakutosha  lakini nina amini tutashinda a nazo na tutarudi na medali "alisema

Naye kocha mchezaji wa timu hiyo David Saimoni  alisema kuwa wakati wanaenda kuiwakilisha nchi katika mashindano haya awajapata msaada wowote kutoka serikali hivyo wameiomba serikali kuwapa msaada na kuukumbuka mchezo huu kama vile wanavyokumbuka  na kuthamini mchezo mpira wa miguu.

"Tunaiomba serikali iukumbuke na mchezo huu iweze kuupa ruzuku kama vile inavyotoa kwa michezo mingine kama mpira wa miguu,katika mashindano haya atujapewa  msaada wowote  kutoka serikali ila tunaenda kuiwakilisha nchi sisi tunachoomba watukumbuke na sisi tunamashindano mwezi wa tisa tulikuwa tunaomba msaada wao"alisema 

Alitaja wachezaji wanaoenda kushindana katika mchezo huu kuwa ni Danny Mkaima,Erick Kaguri ,Ramadhani Msafiri  pamoja na David Samson 

Akibainisha kuwa wanapoenda katika mashindano haya wanaimani watakuja na ushindi mkubwa kwani wamejiandaa vyema na wanaenda kushindana na sio kutalii ivyo wanaimani watakuja na ushindi.

Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates