BREAKING NEWS

Friday, July 8, 2022

WATOTO ZAIDI YA 4000 WAFANYIWA VITENDO VYA UKATILI MKOANI ARUSHA



Mkuu wa wilaya ya karatu   Dadi Kolimba akiongea sherehe za maathimisho ya zoezi la mashindano ya uandishi wa insha kwa kupinga mimba na ndoa za utotoni ngazi ya mkoa

 Na Woinde Shizza ARUSHA 


 
Jumla ya watoto 4365 wa mkoa wa Arusha wamefanyiwa vitendo vya ukatili vikiwemo vya ulawiti na ubakaji 1174  kwa mwaka 2022.

Akizungumza katika sherehe za maathimisho ya zoezi la mashindano ya uandishi wa insha kwa kupinga mimba na ndoa za utotoni ngazi ya mkoa kwa wanafunzi wa shule za msingi zilizoandaliwa na shirika la word vision Tanzania,  afisa ustawi wa jamii mkoa wa Arusha Daniel Kasikiwe alisema kuwa katika mkoa wa Arusha halmashauri ya jiji la Arusha ndio inaongoza kwa vitendo hivyo vya ukatili .



Alisema lengo kuu la shindano hilo ni kupinga mimba na ndoa za utotoni ambazo huathiri safari ya masomo kwa watoto wa kike na kushindwa kufikia ndoto zao katika maisha.


Alisema mwaka 2022 kwa Mkoa wa Arusha  watoto waliofanyiwa ukatili wa kijinsia 4356 ambapo alifafanua kwa halmashauri ya jiji la Arusha ndio linaongoza kwa vitendo hivyo ambapo jumla ya matukio 2140 ya ukatili yamefanyika   ambapo kati yao matukio ya ukatili wa kingono yakiwa 774.


Alisema halmashauri iliofata ni ya Meru ambapo kulikuwepo na jumla ya matukio 721 ya ukatili wa kijinsia ambapo kati yake matukio ya ubakaji na ulawiti yakiwa 95,katika halmashauri ya Arusha DC  matukio ya ukatili yalikuwa 651 kati ya hayo matukio  matukio ya ubakaji na ulawiti ni 134,wilaya ya  karatu matukio ya ukatili yalikuwa 365 kati yake matukio ya ulawiti na ubakaji ni 102,wilaya ya Longido matukio ya ukatili yalikuwa 98 kati yake matukio saba  yalikuwa ya ukatili wa kingono  katika halmashauri ya Monduli  matukio ya ukatili wa kingono yalikuwa 209  ambapo kati yake  matukio ya ukatili wa kingono yakiwa 14




Akiongea kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Arusha John Mongela mkuu wa wilaya ya karatu   Dadi Kolimba  alisema kuwa  Shindano hili la insha litasaidia kuwajenga watoto wa kike kutokudanganyika kuingia katika mitego ya kupata mimba pamoja na ndoa za utotoni kwa ajili ya ustawi wa mkoa na Taifa kwa ujumla



Alisema kuwa  ili kupambana na tatizo hilo serikali ya Mkoa imekuwa ikiendelea na jitihada mbalimbali za kupambana kupunguza au kumaliza kabisa tatizo hilo kwa kukaa vikao na wadau mbalimbali wa elimu,waalimu,wazazi pamoja na wanafunzi wenyewe.


 


Kwa upande wake meneja wa shirika la Word vision  mkoani Babati  Gloria Mashingia alisema kuwa  jumla ya wanafunzi 5000 wameshiriki  shindano hilo 

la uandishi wa insha  kutoka katika shule 47 za mkoa wa Arusha.


Alisema kuwa katika shindano hilo  washindi katika kumekuwa na washindi kutoka  ngazi ya Wilaya,Mkoa pamoja na Kitaifa ambapo alifafanua kuwa wote walioshinda katika ngazi ya mkoa wataenda kushiriki   katika mashindano hayo ngazi ya Taifa


Alisema kuwa katika mashindano haya washindi wote waliondoka na baiskeli pamoja na kitita cha fedha taslimui ambapo pia ali wataka walimu kama walezi wakuu wa vijana kuendelea kuwapa wanafunzi elimu 




Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates