BREAKING NEWS

Tuesday, July 12, 2022

ZAIDI YA WANARIADHA 2000 KUTOKA HAPA NCHINI NA NJE YA NCHI KISHIRIKI MBIO ZA NGORONGORO MARATHON

 


 

 

Jumla ya wanariadha 2000 kutoka Tanzania na nje ya nchi wanatarajia kushiriki katika mbio za Ngorongoro half marathon zinazotarajiwa kutimua vumbi September 11 mwaka huu katika wilaya ya Karatu mkoani Arusha.


Akizungumza na waandishi wa habari, baada ya kutangaza Uzinduzi wa mbio hizo, Mkurugenzi wa taasisi ya michezo ya Meta, ambao ndio waandaji,  Meta Petro alisema wamefungua fursa ya usajili ili kutoa nafasi kwa wanariadha kuanza kujiwekea nafasi ya ushiriki katika mbio hizo za kimataifa.


Alisema kuwa wanatarajia wanariadha zaidi ya  2000 kushiriki katika  mashindano hayo, kutoka nchi mbali mbali ikiwemo za Kenya, Uganda na Rwanda na wenyeji Tanzania bara na visiwani ambao wamekuwa wakisumbua kutaka kujua mbio zinafanyika lini huku wakionyesha Nia ya kushiriki.


"Kama unavyojua mbio zetu huwa tunafanya mwezi April lakini kutokana na baadhi ya changamoto zilizokuwa nje ya uwezo wetu  tuliamua kuhairisha Hadi mwezi September lakini kipindi hicho chote wako wanariadha hasa wa nje ambao hawakuweza kupata taarifa za kuhairisha kwetu, hivyo rasmi sasa tunawaalika waje kushiriki mbio hizi ambazo zimekuwa za kihistoria nchini Tanzania na viunga vyake.

 Meta alisema kuwa katika mbio hizo ambazo zinalenga kutangaza utalii wa Tanzania kwa kumuunga mkono Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania mama Samia Suluhu Hassan, wameandaa zawadi mbali mbali kwa waashiriki wote na washindi  ikiwemo medali, t-shirt na fedha taslim kwa washindi wa kwanza 15.



Alisema  gharama ya usajili katika mbio hizo ni 35,000, tu ambayo italipwa na mshiriki na kuchagua umbali atakaopenda kukimbia.

alisema mbio hizo zitashindanisha wanariadha kwa umbali wa kilomita 21, 10 na tano kwa wale wa kujifurahisha ambao wote wataufaidi utalii wa Nyani na Tumbili walioko geti kuu la Ngorongoro eneo pa kuanzia mbio kabla ya kukutana na burudani za kila aina katika eneo la kumalizia mbio ambayo ni Mazingira bora ulioko katikati ya mji wa Karatu.


Kwa upande wake mwakilishi wa kampuni ya market access, George Damian alisema kuwa wameamua kudhamini mashindano hayo ili kuyaongezea thamani.  

"Hizi mbio ni kubwa kwa hapa Tanzania hivyo tumeona tuije tuongeze nguvu ya maandalizi ambayo tutaifanya kwa kiwango cha kimataifa kutokana na washiriki wanaokuja kukimbia ili kuzivutia zaidi na kutengeneza mabalozi wa nje ya nchi"


Nae katibu wa chama Cha riadha mkoa wa Arusha, Rogath Steven alisema kuwa wameungana na waandaaji wa mbio hizo ili kufanikisha kuvuna wanariadha wenye vipaji ambao watasaidia mkoa na nchi kwa ujumla kuwa na akiba na vipaji.


"Mashindano haya yamekuwa na faida kubwa kwetu, kwani yanatukutanisha na vipaji vipya kila Mara za wanariadha ambao tumekuwa tukiwatumia katika kukuza na kuwaonyesha fursa ya kuwaendeleza lakini pia kupata wanariadha wapya watakaotuwakilisha kitaifa na kimataifa"


Rogath alitumia nafasi hiyo, kuwaalika wanariadha wote kushiriki mashindano hayo, pia vijana chipukizi wanaotaka kuonyesha vipaji vyao kutoka maeneo mbali mbali nchini.

"Wanariadha wanaokuja kushiriki hapa ni wale chipukizi na wataalamu hivyo niwaite vijana wote na watoto wanaojiona wanavipaji vya mbio waje watuoneshe na watuachie kazi ya kuwaendeleza kupitia programe zetu mbali mbali 



Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates