BREAKING NEWS

Wednesday, July 27, 2022

QWIHAYA AMUAHIDI WAZIRI MAKAMBA KUPELEKA NGUZO ZA UMEME NKASI

 



 
Mkurugenzi wa Kampuni za Kuzalisha Nguzo za Umeme ya Qwihaya,  Leonard Mahenda akiwa na Waziri Wa Nishati Mheshimiwa January Makamba wakiwa ziarani Nkasi kutatua kero ya umeme kwa wananchi

Mkurugenzi wa Kampuni za Kuzalisha Nguzo za Umeme ya Qwihaya,  Leonard Mahenda akiwa na Waziri Wa Nishati Mheshimiwa January Makamba wakiwa ziarani Nkasi kutatua kero ya umeme kwa wananchi

Mkurugenzi wa Kampuni za Kuzalisha Nguzo za Umeme ya Qwihaya,  Leonard Mahenda akiwa na Waziri Wa Nishati Mheshimiwa January Makamba wakiwa ziarani Nkasi kutatua kero ya umeme kwa wananchi


Na Fredy Mgunda, Nkasi

Mkurugenzi wa Kampuni za Kuzalisha Nguzo za Umeme ya Qwihaya,  Leonard Mahenda ameahidi kupeleka nguzo za umeme katika kijiji cha Kilando, Jimbo la Nkasi, Mkoani Rukwa.


Mahenda anayejulikana kwa jina la Qwihaya ametoa ahadi hiyo wakati wa ziara ya Waziri wa Nishati, January Makamba baada ya wananchi kuomba kuletewa nguzo za umeme.


Kutokana na hali hiyo, Waziri Makamba alimuomba Qwihaya kupeleka nguzo kwa sababu yeye ni mdau wa bidhaa hiyo licha ya kuwa, ni mkandarasi jimboni humo.


“Nimemuahidi Mh Waziri Makamba kuwa tutapeleka nguzo za umeme bure, sisi ni wadau wakubwa na lazima tumuunge mkono mama yetu  Rais Samia Suuhu Hassan za kueleka umeme kwenye vijiji,” amesema Qwihaya.


Awali Waziri Makamba aliwahakikishia wananchi wa Jimbo la Nkasi kuwa Serikali itapeleka umeme katika vijiji vyote 27 vilivyobaki.

Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates