BREAKING NEWS

Wednesday, July 20, 2022

SERIKALI YAOMBA KUTENGENEZA MPANGO WA KUTOA MASHINE ZA EFD BURE



 Serikali imeobwa  kutengeneza mpango mkakati  kwa ajili ya wafanyabiashara utakao wawezesha kuwapatia mashine za kieletroniki(EFDs)  bure ili kuweza  kuweza kutumia mashine hizo  ambapo kwa kufanya hivyo itasaida kuongeza na kukuza mapato ya taifa nchini.

Kwakufanya hivyo kutasaidia wafanya biashara wengi kuwa nazo kitu ambacho kwa sasa hawana kutokana na gharama kubwa  ya ununuzi wa mashine hiyo hata kusababisha wafanyabiashara wengi kukwepa kutoa risiti kwa sababu hawanapesa ya kwenda kununua

 katibu mwenezi wa chama cha Ada –tadea  Taifa Zuberi Mwinyi alipokuwa akiongea na vyombo vya habari ambapo alibainisha kuwa serikali imekuwa inapoteza mapato mengi kutokana na wafanya biashara wengi kutotoa risiti kwakukosa mashine hizo za EFDs kutokana na mitaji yao kuwa midogo ingawa biashara zinaendelea

Alisema kuwa gharama za mashine hizo ni kubwa sana kwani kwa mashine moja inapatikana kwa kiasi cha shilingi laki nane (800000) jambo ambalo kwa mfanyabiashara mdogo inakuwa ngumu kununu mashine hiyo.

Alifafanua kuwa iwapo serikali itatoa bure mashine hizo kila mfanyabiashara ataweza kuichukuwa na kuiatumia na kama itashindikana kutoa bure basi wapunguze gharama za utoaji wa mashine hizo  ,gharama ambazo watazipanga ziwe  rafiki kwa kila mfanyabiashara na aweze kuzimudu.

Aidha aliwataka  mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) kutoa elimu kwa ya kutosha kwa wafanya biashara na wasiishie  kutangaza kuwa wanatoa elimu wakati wamekuwa hawafanyi hivyo kwa vitendo kama wanavyosema ,huku akiongeza uwa elimu ya kutosha ikitolewa pia itasaidia wafanyabiashara kujua umuhimu wa kulipa kodi .

Alisema kuwa iwapo mashine hizo zitatolewa zitolewe katika kila sekta ikiwepo ya usafirishaji mfano daladala zote ,mabasi makubwa ya usafirishaji mikoani,wamachinga ,wenye maduka, ikiwemo wa mabango, na pindi wanapopewa wakipangiwa viwango vya siku  itasaidia kukusanya fedha nyingi

Aidha pia aliwataka maafisa wa TRA wanapotembea katika mitaa mbalimbali kukusanya kodi ya mapato wawashirikishe na viongozi wa mitaa hilo ili kuweza kurahisha zoezi hilo ,kwani viongozi hao ndio wanajua wafabiashara waliopo  katika mitaa yao .

Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates