Ticker

6/recent/ticker-posts

MONABAN YATOA MSAADA KWA WAATHIRIKA WA MAAFA HAI

DSCF2880Mkurugenzi wa kiwanda cha kuzalisha unga kilichopo jijini Arusha Bw.Philemon Mollel akimkabidhi Mkuu wa wilaya ya Hai Mh.Novatus Makunga msaada wa Tani nne za unga  wenye thamani ya shilingi Milioni 4.2,baada ya wilaya yake kupata maafa yaliyotokana na mvu zilizoambatana na upepo mkali na kusababisha badhii ya watu kukosa nyumba za kuishi
DSCF2878Mkurugenzi wa kiwanda cha kuzalisha unga Arusha Philemon Mollel akiongea mbele ya wanakijiji(hawapo pichani)namna alivyoguswa na maafa hayo yaliyopelekea kutoa msaada huo huku kiwataka wafanyabishara,makampuni,watu binafsi kujitokeza kuwasaidia waanga wa maafa hao,mbali na msaada huo wa tani nne za unga pia alitoa shilingi Milioni moja kwaajili ya waanga
DSCF2861
DSCF2857Mkuu wa wilaya ya Hai Mh.Novatus Makunga akiwa na ugeni mzito kutoka kampuni ya Monaban ofisini kwake,lengo la ugeni huo nikutoa msaada wa chakula kwa waathirika wa maafa ya mvua
DSCF2858Mkurugenzi wa Monaban kushoto Philemon Mollel akiongelea namna alivyoguswa na maafa hayo ambayo yalisababisha baadhi ya watu kukosa makazi ,
DSCF2866Kina mama ambao ndio waathirika wa kubwa wa maafa hayo wakisubiria zoezi la kugawiwa chakula cha msaada
DSCF2870Mtendaji wa kijiji Bi.Trea Ramadhani akitoa shukrani zake za dhati kwa mmiliki wa kiwanda cha kuzalisha unga kilichipo Arusha
DSCF2872Afisa Tarafa Masama Bw.Nsajigwa Ndagile akisoma taarifa ya madhara yaliyotokana na mvua hiyo kuwa ni pamoja na kuezuliwa kwa mapaa ya nyumba,kubomolewa kwa kuta za nyumba na kuharibiwa kwa mazao hasa migomba hali iliyosababisha baadhi ya kaya kukosa mahali pa kulala hivyo kujihifadhi kwa majirani
DSCF2874Wanakijiji wakishuhudia msaada ulioletwa kijijini kwao
DSCF2882Mkuu wa wilaya Novatus Makunga akimkabidhi msaada uliotolewa na kampuni ya Monaban ,mtendaji wa kijiji cha  kwa sadala Bi.Trea Ramadhani msaada uliogharimu zaidi ya milioni 4,kushoto kaimu mkurugenzi Bw.Zabdieli Moshi
DSCF2883Mkuu wa wilaya ya Hai Mh.Novatus Makunga akitoa shukrani zake za dhati kwa mmiliki wa kiwanda cha Monaban kwa kuweza kuwaletea chakula cha msaada na kuwataka makampuni,mashirika na watu binafsi kuiga mfano wa Monaban kwa kuwasaidia waanga wa maafa yaliyotokana na mvua zilizoambatana na upepo mkali na kusababisha watu kukosa makazi hivi karibuni ktika wilaya yake
DSCF2886Mama ambaye ni muathirika wa maafa hayo akitoa shukurani zake kwa mkurugenzi wa kampuni ya Monaban kwa kuweza kuwakumbuka kipindi cha shida na kudai kuwa akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli
Nyumba ya familia ya Bibi Aziza Mohammed baada ya kuezuliwa paa
Bibi Aziza Mohammed kama anavyooneka katika picha baada ya mvua kusababisha mafaa makubwa kwake iliyosababisha yeye kuishi chooni na mjuuku wake
DSCF2862DSCF2865Wanakijiji wakiwa wanashusha mifuko ya unga ndani ya gari

Post a Comment

0 Comments