Ticker

6/recent/ticker-posts

DMZV YAFANYA SHEREHE YA JUBILEE YA MIAKA 25 YA KKKT MWANZA

Askofu mkuu wa Dayosisi ya Mwanza Ziwa Victoria (DMZV) Andrew Gulle kabla ya kufunua jiwe maalum la Jubilee alikata utepe kuashiria safari ya maadhimisho hayo kuanza rasmi, ambapo kilele chake kitakuwa tarehe 31 Agosti, 2014.  
Jiwe la jubilee.
Maaskofu waalikwa toka makanisa mbalimbali kanda ya ziwa na Tanzania kwa ujumla.
Baada ya tukio la kuzindua jiwe la Jubilee Maaskofu na mamia ya waumini walielekea kwenye jengo la Kanisa kuu la Mwanza kwaajili ya kulizindua.
Kabla ya Uzinduzi wa kanisa la Imani KKKT Mwanza historia ya ujenzi wa kanisa hadi kukamilika ilisomwa naye Bw. Serafin Kimaro. Jumla ya shilingi bilioni moja na milioni 500 zimetumika kukamilisha ujenzi huo uliotumia miaka takribani 13 hadi kukamilika.
Akishuhudiwa na mamia ya waumini na viongozi wa makanisa mbalimbali Kanda ya ziwa na mikoa mingine nchini ukafika wakati sasa wa mgeni rasmi Mkuu wa KKKT Askofu Dr. Alex Geaz Malasusa kukata utepe kuzindua kanisa la KKKT Imani Makongoro Mwanza. 

Post a Comment

0 Comments