WAFANYA BIASHARA WA MKOANI MANYARA WATESEKA KWA KUKOSA OFISI YA TRA MKOANI KWAO

Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Manyara, imeiagiza Mamlaka ya mapato nchini (TRA) mkoani humo, kufungua ofisi kwenye Wilaya za Simanjiro na Hanang’ ili kuwawezesha wafanyabiashara walipie ushuru na kodi wakiwa eneo la karibu.
 
Imeelezwa kuwa, wafanyabiashara wa wilaya za Simanjiro na Hanang’ wanakabiliwa na tatizo la kutokuwa na ofisi za kulipia mapato yao, hivyo kulipia kwenye ofisi za TRA za mikoa ya Arusha na Kilimanjaro na wilayani Mbulu.
 
Akizungumza kwenye mkutano wa 20 wa kamati hiyo mjini Babati juzi, mkuu wa mkoa huo, Elaston Mbwilo alisema ofisi hizo zinatakiwa kufunguliwa kwenye miji ya Mirerani wilayani Simanjiro na Katesh wilayani Hanang.’
 
Mbwilo alisema maeneo hayo yanatakiwa kuwa na ofizi za TRA ili kukusanya mapato yatakayowezesha mkoa huo kuingia mapato nchini, kuliko hivi sasa kwani baadhi ya wafanyabiashara wanalipia nje ya mkoa wake.
 
Alisema mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Hanang, Felix Mabula aliahidi kutoa chumba kwenye jengo la hamashauri tangu Julai mwaka jana, wakati TRA wanajipanga na utaratibu wa kupata ofisi za kudumu.
 
“Pia kwenye wilaya ya Simanjiro nao tuliwashauri kutafuta eneo la muda ili kuongeza mapato kwa kuwa baadhi ya wafanyabiashara wake wanalipa kodi mkoani Arusha na Kilimanjaro,” alisema Mbwilo.
 
Kutokana na hali hiyo waliazimia Katibu Tawala wa mkoa aandike barua kwa Kamishna wa TRA kuomba kufunguliwa ofisi kwenye wilaya hizo na kueleza nanma wanavyopoteza mapato kutokana na kukosa ofisi katika maneo hayo.
 
Hata hivyo, baadhi ya wafanyabiashara wa miji ya Mirerani na Katesh, walilalamikia ukosefu wa ofisi, kwani watumishi wa TRA huwa wanawavamia na kutaka mapato hivyo wangekuwa na ofisi wangetoa ushirikiano mkubwa.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia