CONTAGIOUS KUZINDUA KAMPUNI YAO RASMI

 
Kundi la muziki la Contagious lenye maskani  yake jijini Arusha limejipanga kujitanua zaidi  kimataifa ambapo safari hii limejipanga kuanzisha kampuni ya kusimamia kazi zao kikamilifu.

Akihojiwa na gazeti hili kiongozi mkuu wa kundi hilo,Njara Rasolomanana alisema kuwa katika mojawapo ya mikakati yao ni kutangaza kazi zao kitaifa na kimataifa.

Alisema kuwa wako katika mkakati wa kuanzisha kampuni ambayo itakuwa na jukumu la kusimamia kazi zao kwa ufanisi pamoja na kuwaunganisha na mataifa mbalimbali.

Bila kutaja hadharani jina la kampuni hiyo alisema kwamba malengo ya  kampuni hiyo itakuwa ni pamoja na kusimamia  makundi mengine ya muziki ambayo ni washirika wao yaliyopo katika nchi za Madagascar na Finland.

Njara,ambaye ni raia wa nchini Madagascar alisisitiza ya kwamba kwa sasa wanaendelea na kazi ya kuibua vipaji vya wanamuziki wachanga waliopo ndani ya kundi lao.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia