Ticker

6/recent/ticker-posts

MAKOFULI UMELALAL MBONA VIWANGO VYA BARABARA ZINAZOTENGENEZWA HAPA NCHINI KIKO CHINI

 
 
Serekali imesema pamoja na juhudi zinazofanywa nayo bado ufuatilia na ukaguzi unaofanyika mara kwa mara umebaini kuwa viwango vya utekelezaji wa kazi za matengenezo ya barabara kiko chini ya matarajio ya ofisi ya waziri mkuu Tamisemi na bodi ya mfuko wa barabara na wadau wengine.

Huku halmashauri hazifikii malengo yaliowekwa kwa mwaka hali hii haikubaliki kwani imekuwa ikirudisha nyuma dhamira ya serekali ya kuwa na barabara zinazopitika muda wote wa mwaka na kuwawezesha wakulima kuyafikia masoko yote ya mazao.

Akifungua mkutano wa pili wa wadau wa mfuko wa barabara unaotathmini ya utendaji kwa mwaka wa fedha 2013-14 waziri wan chi tamisemi Hawa Ghasia alisema kuwa hatua hiyo ni muhimu ya kupanga mikakati itakayowezesha sekta ya barabara kuboresha maisha ya watanzania.

Ghasia alisema kuwa moja ya majukumu yao makubwa ni kuhakikisha miradi yote ya ujenzi inakidhi viwango,matakwa na azma ya serekali pamoja na washirika wake wa maendeleo na kuwa watendaji hao na wenyeviti,mameya,watatumia mkutano huo wa siku 5 kujiwekea malengo na mikakati kwa mwaka wa fedha ujao kufikia malengo tuliyokusudia.

“Rasilimali tulizonazo zitumike ipasavyo ili thamani ya fedha iweze kupatikana na kuleta maendeleo watakaoshindwa kwenda na kasi hii waanze kujiweka pembeni mapema kwani mikakati tulioweka itazisaidia wakala wa barabara(TANROADS)na mamlaka za serekali za mtaa kutumia fedha kwa ufanisi uwazi na uwajibikaji”alisema waziri Ghasia

Waziri alizitaka Halmashauri zihakikishe zinasimamia kikamilifu taratibu za utoaji wa zabuni na mikataba iainiwe kwa wakati huku hatua za kinidhamu zichukuliwe kwa watendaji wote wanaothibitika kusababisha kazi mbovu na upotevu wa fedha za mfuko wa barabara.

Kwa upande wake naibu katibu mkuu  ofisi ya waziri mkuuTamisemi Alphayo Kidata alisema kuwa kumukuwa ongezeko la mtandao wa kilomita za barabara katika mamlaka za serekali za mitaa kufikia km96,096 huku jmla ya km56,624.69 ziliingizwa kwenye sheria za baraya mwaka 2007 huku kutokana na uhaba wa fedha ni km30,000 sawa na31% ndizo hutengenezwa kwa mwaka.

Alphayo alisema kuwa fedha iliyopangwa kwa mamlaka ya serekali za mitaa kwa mwaka2012-13 ni b127.6 fedha hizi zilipangwa kwa matengenezo ya km30,402 hadi kufikia mwishoni mwa robo ya tatu miaka hiyo ni kiasi cha tsh48.29 zilikuwa zimepelekwa kwenye halmashauri zote kwa ajili ya matengenezo ya barabara huku kiasi tsh.26.27 sawa na aslimia54 zilikuwazimetmuka kwa matengenezo ya km11,527.

Alisema kuwa jumla ya bilion41.87 zilivuka robo ya nne ya mwaka wa fedha kutoka na hali hii na uchelwaji wa kusaini mikataba ndiko kumefanya halmashauri nyingi kushindwa kufikia malengo ya wadau wa mfuko wa barabara.

Imeonekana kuwa ufuatiliaji wa zabuni za serekali imekuwa ndiyo chanzo cha uchelewaji na kuvuka kwa fedha za miradi hiyo kwa kutaka mikataba kwanza baada ya fedha kufika huku kumekuwa kukichelewesha miradi ya barabara sehemu mbali mbali humu nchini na kuleta viwango duni vya barabara hali inayodumaza maendeleo,

Post a Comment

0 Comments