|
Naibu
Waziri wa Wizara ya Kilimo na Maliasili wa Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar Mhe. Mtumwa Kheir Mbarak akihutubia wakati wa sherehe fupi za
ufunguzi wa ofisi hizo za Tanzania Horticultural Association (TAHA) |
|
Mkurugenzi wa TAHA, Bi Jacqueline Mkindi akisema neno la ufunguzi kwa Mh. Mtumwa Kheir Mbarak na wageni waharikwa wakati wa sherehe hizo za ufunguzi wa Ofisi za TAHA-Zanzibar |
|
Moja ya mashamba darasa ya TAHA yaliyopo eneo la Donge, Wilaya ya Kaskazini Unguja. |
|
Wakulima
wanaojishughulisha na kilimo cha Mazao ya horticulture wakiwa katika
moja ya Warsha zilizoandaliwa na TAHA masaa machache kabla ya ufunguzi
wa ofisi hizo kisiwani hapo. |
|
Baadhi
tu ya pilipili bora zinazolimwa na wakulima wanachama wa TAHA, mazao
haya yenye afya ni matokeo ya elimu za kilimo bora zinazotolewa na
wataalamu wa TAHA visiwani humo. |
|
Hili
ni soko la Darajani Zanzibar, ni baadhi tu ya maeneo ambayo bidhaa za
wakulima wa horticulture Zanzibar upelekwa na kuuzwa kwa ajili ya kukizi
haja za soko la ndani. |
|
Mkurugenzi
wa TAHA akiteta Jambo na Mtaalamu wake kwa upande wa Visiwani Mzee Biwi
wakati alipotembelea moja ya mashamba ya tikiti maji ya wakulima ambao
ni wanachama wa TAHA. |
|
Wataalamu
kutoka Finland ambao ndio wawezeshaji wa shughuli za TAHA Zanzibar
wakitazama moja ya shamba la Matikiti maji la moja ya vikundi wanachama
wa TAHA. |
Ukiwa na swali hoja na maoni ingia hapa uwasiliane nao leo TAHA
Taasisi
kilele ya TAHA inayoundwa na wakulima wanaojishughulisha na kilimo cha
'horticulture' nchini Tanzania hatimaye imefungua rasmi ofisi zake kuu
katika visiwa vyenye marashi ya karafuu Zanzibar. Ufunguzi wa ofisi hizo
zilizo mtaa wa Kikwajuni kwenye Jengo la mfuko wa barabara ulitanguliwa
na ziara fupi ya kutembelea maeneo ambayo Taasisi hiyo imeanzisha
mashamba darasa na kusajili vikundi vya wakulima ili waweze kufaidika
kwa karibu zaidi na ushauri wa kiufundi katika masuala ya kilimo cha
'horticulture' hali kadhalika masoko ya kuuza bidhaa zao ndani na nje ya
nchi.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia