UCHAGUZI WA UDIWANI ARUSHA KUFANYIKA JULY 14,POLISI KULINDA VITUO VYA KUPIGIA KURA

 Mkurugenzi wa jiji la Arusha Sipora Liana akiwa anaongea na waandishi wa habari kuhusiana na uchaguzi wa udiwani  jijini hapa
 picha chini na juu waandishi wa habari wakiwa wanasikiliza mkurugenzi wa jiji la Arusha



Alisema kuwa kwa sasa maandalizi yaote yamekamilika na taratibu zote za kutangaza tena kwa wasimamizi ,wasimamizi wasaidizi pamoja na makarani zimekamilika na pia wameshapatiwa mafunzo kwa ajili ya wasimamizi hawa yameanza jana na yataendeshwa kwa muda wa siku tatu.



Aliwataja wagombea kutoka kata ya Kimandoku ni pamaja Edna  Saul (CCM) pamoaja na Rayson Ngowi kutoka (CHADEMA) ,aidha alisema kuna jumla ya vituo 136 vya kupigia kura ambapoalisema kaloleni kuna vituo 27,elerahi 55,kimandolu 39, na kata ya themi vituo 15 .

Alisema kuwa jumala ya wapiga kura sitini elfu mia moja ishirini na tatu (60,123)wanatakiwa kupiga kura  kaloleni itakuwa na wapiga kura 12,636,Elerai  watakuwa wapiga kura 23,797,kimandulu 17,294 na Themi wapiga kura 6,396 aidha alisema kuwa wapiga kura wote wanatakiwa kufika katika vituo mapema kwani kura zitaanza kupigwa kuanzia saa moja asubui hadi saa kumi jioni ambapo baada ya hapo watafunga na askari watakuwa wanalinda vituo vyote.

Aliwataka wananchi kutimiza wajibu wao wa kupiga kura kwani zoezi hili ni muhimu huku akiwahakikishia kuwa usalama utakuwepo wa kutosha  wakati wa kupiga kura na aliwataatharisha wananchi kuwa endapo mtu yeyete atawasumbua wakiwa katika eneo la kupigia kura  watoe taarifa kwa askari aliopo karibu yake ili achukuliwe hatua za kisheria.


''ninawaomba kutowazingatia  wanaopita kuwaaambia msijitokeze kwenda kutumia haki yenu ya msingi za kikatiba kuwachagua viongozi wenu  pia napenda kuchukuwa nafasi hii kuwatakia wananchi wote wa jiji wa arusha uchaguzi mwema''alisema Sipora.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia