LEMA AMUAHAIDI MKURUGENZI WA JIJI LA ARUSHA KUMPA USHIRIKIANO WA KUTOSHA
WAKATI ushindi wa kishindo wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA) jijini Arusha ukimweka pabaya Meya wa Jiji la Arusha, mazito
mengine yameibuka baada ya Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Sipora Liana,
kutoboa siri kubwa.
Mbele ya madiwani wapya wa CHADEMA wakiongozwa na Mbunge wa Arusha
Mjini, Godbless Lema, Liana alisema alikuwa anafikiria ‘kukimbia’
kutokana na hali tete ya usalama kugubika jiji hili.
Katika kikao kifupi cha utambulisho wa madiwani hao wapya, Liana
alisema: “Wakati ninakuja hapa (Arusha) kulikuwa na
taarifa za vurugu
na maandamano, jambo ambalo lilinifanya nifikirie kama hali ingeendelea
kuwa hivyo nitaomba niondoke, lakini nimeridhishwa na utulivu
uliokuwepo jana (juzi),” alisema Mkurugenzi Liana.
Kauli hiyo ilimfanya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, kumweleza
mkurugenzi huyo kuwa hata wao CHADEMA wataendelea kumpa ushirikiano wa
kutosha kuhakikisha kuna kuwapo maendeleo ya wananchi wa jiji hilo, hasa
kutokana na namna alivyoonyesha ushirikiano wakati wa uchaguzi huo.

0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia