LEMA AMUAHAIDI MKURUGENZI WA JIJI LA ARUSHA KUMPA USHIRIKIANO WA KUTOSHA


WAKATI ushindi wa kishindo wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) jijini Arusha ukimweka pabaya Meya wa Jiji la Arusha, mazito mengine yameibuka baada ya Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Sipora Liana, kutoboa siri kubwa.
Mbele ya madiwani wapya wa CHADEMA wakiongozwa na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, Liana alisema alikuwa anafikiria ‘kukimbia’ kutokana na hali tete ya usalama kugubika jiji hili.
Katika kikao kifupi cha utambulisho wa madiwani hao wapya, Liana alisema: “Wakati ninakuja hapa (Arusha) kulikuwa na
taarifa za vurugu na maandamano, jambo ambalo lilinifanya nifikirie kama hali ingeendelea kuwa hivyo  nitaomba niondoke, lakini nimeridhishwa na utulivu uliokuwepo  jana (juzi),” alisema Mkurugenzi Liana.
Kauli hiyo ilimfanya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, kumweleza mkurugenzi huyo kuwa hata wao CHADEMA wataendelea kumpa ushirikiano wa kutosha kuhakikisha kuna kuwapo maendeleo ya wananchi wa jiji hilo, hasa kutokana na namna alivyoonyesha ushirikiano wakati wa uchaguzi huo.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia