Ticker

6/recent/ticker-posts

WAKAZI WA ARUSHA WAENDELEA NA ZOEZI LA KUPIGA KURA


Wakazi wa kata nne za jimbo la Arusha mjini leo(jana)wamepiga kura kwenye uchaguzi mdogo wa marudio baada ya chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA)kuwafukuza madiwani wake kutoka kata za Elerai,Kaloleni,Kimandolu na Themi hali iliyopekea kuitishwa kwa uchaguzi huu mdogo.

Miongoni mwa kata hizo ya Themi uchaguzi umeendelea kwa amani licha ya kasoro mbali mbali zilizojitokea ikiwemo ya watu kutokuta majina yao kwenye ubao wa majina hali liyoleta sintofahamu kwa wakazi wa kata hiyo wakiwemo wagombea kuhoji.

Akihoji suala la utata wa kutokuwepo kwa majina ya wapiga kura akiwemo yeye mgombea wa CUF Lobora Ndarpoi alisema kuwa ameenda sehemu aliyojiandikisha lakini hakukuta jina lake lakini baada ya maelekezo ameweza kupata haki hiyo.

Ndarpoi alisema kuwa hali kama hii itawafanya wananchi kutopiga kura na kupoteza haki yao ya kikatiba huku akiwataka wakazi wa kata hiyo kujitokeza kwa wingi kupiga kura na kutomia haki yao ya kidemokrasia.

Akizungumza kwa upande mwingine Msimamizi msaidizi wa uchaguzi kata ya Themi Bi Eveta Mboya alisema kuwa majina ya wapiga kura yalibandikwa takribani siku 30 na kuwa wananchi walishindwa kuja kuhakiki.

 Eveta alisema kuwa usumbufu kama huu ni wakujitakia kwani kama ungeweza kuja kuhakiki hapa unajua upo kituo gani hili ni tatizo na kuwataka wakazi wa kata hizo na watanzania kwa ujumla wake kujenga mazoea ya kuhakiki majina yao kabla ya siku ya kupiga kura kukwepa usumbufu kama huo.

“uhakiki ni jambo la muhimu ili kukwepa usumbufu wa kutoona jina siku ya kupiga kura kumbe jina lipo kwenye kituo chengine kama huyu hapa jina lipo Engira shule ya msingi yeye kaja Zahanati kama angehakiki usumbfu kama huu asingeupata”alisema Eveta.

Katika hali nyingine Gazeti hili liliwashuhudia baadhi ya vijana wakiwaelekeza wenzao kumpigia kura mgombea mmoja wa chama kimmoja ili aweze kupita katika uchaguzi huo

Hali ya uchaguzi katika kata hizi inaonekana kuwa ya amani huku askari wakionekana kulinda amani hali inayoufanya jiji kuwa kataka hali ya utulivu na Amani wananchi wengi wamekuwa wakiendelea na shughuli zao za mwishi wa wiki.

Katika hali nyingine huko kwenye kata ya Kimandolu kumeonekana hali ya sintofahamu baada ya vijana waliokuwa wakipita wakiwa kwenye gari kukamatwa kwa kujaza gari na kupelekwa kwenye kituo cha polisi.

Akizungumzia hilo kamanda wa polisi mkoani hapa Liberatus Sabas alisema kuwa hao wahausiani na suala la uchaguzi bali wamekamatwa kwa sheria za Trafiki kwa kuzidi abiria kwenye gari badala ya abiria wanaotakiwa.

Post a Comment

0 Comments