Ticker

6/recent/ticker-posts

Mbio za kuruka vihunzi zinavyopotea kwa kasi



 

 Mbio za kuruka vihunzi au (hurdles), ni mbio ambazo zimeadimika kama siyo kupotea kwa kasi hapa nchini pengine hata kusahaulika kabisa katika masikio ya walio wengi.
Mbio hizi za vihunzi ambazo huwa na vizuizi vya chuma, mshiriki  huruhusiwa kukimbia kuanzia umri wa miaka 15 na kuendelea na huwa na tofauti kati ya wanawake na wanaume.
Katika mbio hizi kwa wanawake huwa na mbio zao na wanaume pia huwa na mbio zao, ambapo wanawake huruka mita 3.5 huku wanaume wakiruka mita 4 kamili na kila safu au barabara ya kukimbilia ambazo ni njia nane kila mchezaji hupaswa kuruka vihunzi 6 mpaka mwisho.
Idadi kamili ya vihunzi ambavyo hupangwa uwanjani kabla ya kukimbia huwa ni 40 ambavyo hupangwa katika njia nane za kukimbilia huku ikitegemea ukubwa wa uwanja na mistari iliyochorwa.
Umbali wa kila kihunzi hadi kihunzi ni mita 7 kwa pande zote mbili yaani kwa upande wa wanaume na wanawake, lakini katika mchezo huu kinacholalamikiwa zaidi ni gharama za vifaa vya mbio hizi.
Vifaa vya mchezo huu ni adimu na havipatikani kwa urahisi, hapa nchini vifaa vya mchezo huu vipo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam pamoja na Chuo cha Michezo kilichopo mkoani Arusha.
Vihunzi ni vyuma vigumu sana hivyo endapo mkimbiaji atakosa umakini kwa kugonga maeneo ya magoti anaweza kupata kilema.
Mbio hizi za kuruka vihunzi ni tofauti na mbio za kawaida kwa kuwa katika ukimbiaji wa mbio hizi nguvu ya ziada inahitajika kutokana na mpangilio wa vihunzi anavyowekewa mkimbiaji wakati wa kukimbia.
Mkimbiaji wa mbio hizi anapaswa kuepuka na vyakula vyenye mafuta mengi kama chips, samli, karanga na vingine vingi ila anashauriwa kutumia mboga mboga, matunda kama machungwa kwa wingi, mapapai, matikiti pamoja na kunywa maji mengi mara kwa mara bila kusahau mazoezi ya mara kwa mara

Post a Comment

0 Comments