Ticker

6/recent/ticker-posts

MAGUFULI AKAGUA MRADI WA MAGARI YA MWENDO KASI DAR


 Muoenekano wa ujenzi wa mradi wa daraja la Kigamboni katika awamu ya kwanza ukiwa umekamilika kwa asilimia 47, katika mradi huo.  Ujenzi huo  utagharimu jumla ya Sh. Bilioni 214,kati ya fedha hizo asilimia 60 zimetolewa na Shirika la Hifadhi ya Mfuko wa Jamii (NSSF). Picha hii imepigwa jana wakati Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli (hayupo pichani) alipofanya ziara ya siku moja  ya kukagua maendeleo  ya ujenzi wa miradi ya Miundombinu hiyo ya jijini Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na ujenzi wa daraji hili.

Picha ya Daraja hilo kama ilivyopigwa kutoka juu inavyoonekana.
 Ujenzi wa barabara unaoendelea katika barabara ya Davis Corner- Vituka - Jet Corner.
  Ujenzi wa baadhi ya Vituo vya mradi wa Mabasi ya mwendo kasi (DART)  barabara ya Morogoro, eneo la Ubungo,Mwembechai na Jangwani vikiendelea.
 Sehemu ya muonekano wa kituo cha mabasi ya mwendo kasi  eneo la Kigamboni.
 Waziri wa Ujenzi Dkt, John Magufuli, (mwenye kofia ya pama) akiongea na  Diwani  wa kata ya Mwenge Dkt. Julian Bujugo (aliemshika begani) wakati ya ziara yake .
Picha ya Pamoja kati ya Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli  pamoja na viongozi waliokuwa katika ziara yake. Picha na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO

Post a Comment

0 Comments