Ticker

6/recent/ticker-posts

CHADEMA WAJIPANGA KULINDA KURA ARUSHA,NASSARI NIPO GADO,MPINGA SIJAJITOA KUGOMBEA UDIWANI


CHAMA cha demokrasia na maendeleo chadema kimesema kuwa kitatumia gamarama ya aina oyote  kulinda kura za uchaguzi mdogo  wa udiwani unaotarajiwa kufanika mapema july 14 mwaka huu katika kata nne za jijini la Arusha .
Haya yamebainishwa na mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema wakati akiongea nagomaa moto   waandishi wa habari kuhusiana na uchaguzi wa udiwani unaotarajiwa kufanyika mapema jul 14 mwaka huu katika kata nne ambazo ni  kalole ,Themi,Kimandolu pamoja na Elerai.
Alisema kuwa katika kipindi hichi cha uchaguzi wabunge wapatao 16 watakuwepo kwa ajili kuimarisha ulinzi wa kura pamoja na vijana wa chadema ikiwa ni pamoja na vikosi maalumu wakiwemo redbrigedi,QX1 hakuna matata na FB6 ngoma moto .
Aidha lema alisema nguvu kubwa zaidi wanatarajiakuweka haswa maeneo ambayo walikuwa wanapata wasiwasi wa kuibiwa kura zao ambapo alisema kuwa wamejipanga kuchukua kata zote kwa asilimia zaidi ya 80% ambapo alibainisha kuwa kimandolu kwa asilimia 92%,kaloleni  82% na Elerai asilimia 82 %.
Wakati huo huo mbunge wa jimbo la Arumeru mashariki Joshua Nassari  ambaye ameingia jijini hapa kutokea katika hospitali ya muhimbili kwa matibabu alisema kuwa ingawa amepigwa maeneo mbalimbali mwilini mwaka katika maeneo ya sehemu za shingo ,kwenye mbavu  ,mgongo pamoja na kifua lakini anashukuru mungu amepona na amerudi rasmi akiwa na afya bora na kusema kuwa upo tayari kuendelea na mapambano.
"napenda kuwaamba wananchi wangu wa jimbo la Arumeru mashariki kuwa nimerudi kwa nguvu kubwa na tutaendeleza mapambano pale tulipoishia  na pia nawaambia dhambi kubwa kuliko yote duniani ni woga"alisema nassari
Aidha alilishutumu jeshi la polisi vikali kwa kwa kutumia nguvu kubwa  kuzuia mapokezi yake pamoja na kufanya mkutano wa kuongea na wananchi wake katika jimbo lake kwa kigezo kwamba kuna uchaguzi jumapili wa udiwani wa jiji Arusha
"mimi nawashangaa wanatumia nguvu kubwa kuzuaia mkutano badala ya kulinda ualifu na tembo wanaoibiwa kila siku katika hifadhi zetu pamoja na ujambazi wa ungaltd kwa kigezo kwamba kunauchaguzi katika jiji la arusha wakati mimi nafanyia arumeru katika jimbo langu............. kunamusiano gani kati ya arumeru na arusha?".alisema Nassari

Naye mgombea udiwani wa kata ya Elerai Eng.Jeremia Mpinga akikanusha vikali tuhuma za kujiondoa kwenye kinyanganiro cha udiwani wa kata yake alisema kuwa ajajiondoa kugombea  kata hiyo ya elerai kama baadhi ya mitandao ya kijamii na watu wanavyodai .

Alisema kuwa uvumi huo umetokea baada ya mbunge wa ccm Mwigulu Nchemba  kumshawishi yeye kuacha  kugombea na kudai kuwa atapewa ukuu wa wilaya  akijitoa kwenye kinyanganiro hicho kwa kupitia chama cha chadema.
"mimi nipigiwa simu tarehe Juni 12 saa tatu asubui na mwigulu akitaka kuongea na mimi kwa madai kuwa ametumwa na rais kuniuliza nitakacho ili niache kugombea udiwani kupitia chadema lakini alivyokuja kwangu nilimwambia sitaki na meseji za ushaidi ninazo na mbali na ivo nilitoa taarifa polisi  kutokana na swala hilo kwani nilivyomwambia sitaki alinijibu kuwa ccm ndo imekamata dola naiwapo nitafikiria vizuri ni mpigie simu lakini adi leo sijawasiliana nae"alisema Mpinga
Pia mpinga alikiri picha iliyopo kwenye mitandao ni ya kwake akiwa na mwigulu nyumbani kwake lakini alishangazwa maelezo yaliyowekwa na picha hiyo kuwa amejitoa na ajui muda aliyopigwa picha hiyo .
"nilikuwa namueshimu sana nchemba kama mbunge wangu kwakuwa tumetoka kijiji kimoja lakini kwa ushenzi huu aliofanya sitomuheshimu daima "alisema mpinga
Alitoa wito kwa wananchi kujitokeza kujitokeza kupiga kura  kwa wingi kwani yeye ajajitoa kugombea nafasi ya udiwani  kwani anawapenda wananchi wake.

Post a Comment

0 Comments