Ticker

6/recent/ticker-posts

KIMBEMBE BAADA YA BARAZA LA MAWAZIRI KUTANGAZWA TU DR SLAA AHANZA NA MWIGULU ASEMA AMEWEKWA KUIBA FEDHA ZA UCHAGUZI 2015

Dk Slaa Willibrod.
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa amesema Mwigulu Nchemba ameteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Fedha kwa lengo la kupanga mkakati wa kuiba fedha kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 205.

Dk Slaa amesema kwamba baraza la jipya mawaziri lililoteuliwa jana, limejaa viraka na halitakuwa na tija kwa Watanzania.

Akizungunza na gazeti moja  kwa njia ya simu jana  baada ya kutangazwa kwa baraza hilo, Dk Slaa alitoa maoni yake na kusema kwamba baraza lililotangazwa kabla ya kufanya kazi tayari limechoka na halitakuwa na tija kwa Watanzania.

Amesema baada ya kuteua baraza jipya lenye weledi na uzoefu baadhi yao wameteuliwa kwa kubebana.

“Hili baraza halina jipya, halitakuwa na tija kwa Watanzania, tulikuwa tunahitaji baraza ambalo litawasaidia Watazania katika kupata matumaini ya maisha yao magumu waliyonayo sas, lakini kinachoonekana hapa ni viraka vilivyoshonwa  tu na si la kuwanufaisha wananchi,” amesema.

Dk Slaa amesema kwamba uteuzi wa Mwigulu ni kutokana na malengo ya CCM kujinufaisha wenyewe na kutafuta fedha kwa ajili maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

“Yaani Baraza la Mawaziri kubwa sana, sasa tulitegemea pia Rais akifanya mabadiliko apunguze vilevile na baraza, lakini ndiyo kwanza amewarundika,” amesema.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana amesema baraza jipya la linaweza kuleta tija  hasa katika sekta ya elimu kutokana na kumweka Mbunge wa Peramiho, Jenister Muhagama. Source: Tanzania Daima.

Post a Comment

0 Comments