Ticker

6/recent/ticker-posts

MBOWE AITAHADHARISHA CCM JUU YA SEREKALI TATU

Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi,  James Mbatia akizungumza kwenye mkutano mkuu wa chama hicho jana. 

Leticia Ghati na Haji Ambar Khamis jana wamechaguliwa kuwa Makamu Wenyeviti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, katika Mkutano Mkuu wa Nane wa chama hicho uliofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee.
Ghati ambaye amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti (Bara) alikuwa akiwania nafasi hiyo na Anyimike Mwasakalali, Rakia Abubakar Hassan na Danda Juju ambao walijitoa kugombea dakika za mwisho.
Kwa upande wa Ambar Khamis(Makamu Mwenyekiti Bara) alipita bila kupingwa kutokana na kuwania peke yake nafasi hiyo.
Msimamizi wa Uchaguzi huo, Moses Machali ambaye pia ni Mbunge wa Kasulu Mjini, aliwatangazia wajumbe wa mkutano huo kuwa Ghati na Ambar ni wagombea waliokosa upinzani, bila kufafanua sababu za wapinzani wa Ghati kujitoa.
Awali katika ufunguzi wa Mkutano huo, Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe alikitahadharisha Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuacha mpango wake wa kutaka kukwamisha Mfumo wa Muungano wa Serikali tatu uliopendekezwa katika Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Pia CCM kimetakiwa kutambua ya kuwa siku kitakapoondoka madarakani viongozi na wanachama wake wataendelea kuwa katika hali ya usalama na wala hakuna atakayelipiza visasi kwa kushindwa kusimamia umwagikaji wa damu za Watanzania wasiokuwa na hatia.
Akizungumza kwa niaba ya wenyeviti wa vyama vya upizani waliohudhuria mkutano huo alisema: “Serikali tatu siyo sera ya chama chao sisemi kwamba ni lazima wakubali serikali mbili au nne au moja sisemi hivyo, ila kauli kwamba siyo sera yao ni kiashirio kwamba wanaangalia masilahi ya chama na si ya Taifa,” alisema Mbowe huku akishangiliwa na wajumbe wa mkutano huo.
Akitoa salamu za CCM, Mangula alisema hakuhudhuria mkutano huo kwa lengo la kujibu mapigo, bali kuangalia jinsi uchaguzi huo utakavyokuwa na mmoja wa wanachama wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD).
Awali Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia alisema damu za Watanzania zinazomwagika ardhini bila hatia zinatokana na utawala mbovu wa CCM.
“Tunataka maridhiano ya kitaifa, tuzungumze, turidhiane pamoja kwa kuweka masilahi ya Taifa na rasilimali kwanza vyama badaye.” aliongeza
Naye Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi aliwataka wajumbe wa mkutano huo kutumia fursa hiyo kuwachagua viongozi watakaokuwa na taswira ya kuwafikisha mbali katika siasa.
“Wanachama hii ndiyo nafasi pekee ya kuwachagua viongozi bora ambao wamekomaa na wastaarabu watakaowaepusha na migogoro na wenye sura ya utaifa,” alisema Jaji Mutungi

Post a Comment

0 Comments