Ticker

6/recent/ticker-posts

NGORONGORO MARATHON KURINDIMA APRIL 18

 
Mbio za nusu Marathon kilomita 21 za Ngorongoro  zenye lengo la kutokomeza ugonjwa wa Malaria zinatarajiwa kufanyika mnamo tarehe 18 ya mwezi huu wilayani Karatu na kuwashirikisha wakimbiaji nguli kutoka ndani ya nchi na nchi jirani.

Mbio hizo zinazofanyika kwa msimu wa nane ambapo mshindi wa mbio hizo mwaka jana Alphonce Modest nae pia anatarajiwa kutetea ubingwa wake kwenye mbio hizo za mwaka huu.

Kwa mujibu wa mratibu wa mbio hizo Mwta Petro alisema kuwa zawadi zimeboreshwa katika mbio hizo kwa wahsindi wote kwani mshindi wa kwanza atajinyakulia kitita cha shilingi million 1 na laki mbili huku mshindi wa pili akijinyakulia sh.laki sita na watatu sh.laki nne.

Petro alisema kuwa mbio za mwaka huu zitakuwa na mbio za kilometa tano kwa makundi ya wafanyakazi kutoka taasisi mbali mbali na washindi watapata fursa ya kutembelea mbuga ya wanyama ya Ngorongoro huku pia kutakuwa na mbio za kilometa 2.5 kwa vijana na wanafunzi ambao wanaandaliwa kuwa wakimbiaji hapa mbeleni.

“Tunatarajiwa mbio hizo kuwa kubwa hapo baadae kwani zimeonyesha kuwa na mvuto kwa washiriki mbali mbali kutopka ndani na nje ya nchi kwani kwa mwakan huu kumekuwa na wakimbiaji kutoka mataifa ya marekani,Norway na Sweden na nchi za ukanda wa Afrika ya Mashariki na Malawi pia wamethibtisha kushiriki mbio hizi”alisema Meta.

Akawataka wanariadha mbalimbali kuanza kujiandikisha kwani vituo teyari vimeshafunguliwa kwenye mikoa ya Arusha,Manyara,Kilimanjaro na wilayani Karatu huku akiwataja wadhamini wa mbio hizo zilizokuwa zikidhaminiwa na kampuni ya simu za mikononi ya Tigo kuwa ni Kampuni ya vinywaji baridi ya Coca Cola na Zara Charity.

Post a Comment

0 Comments