Ticker

6/recent/ticker-posts

KATIBU WA WAZAZI AWATAKA WANA CCM KUJIUNGA

SAM_3529
Katibu wa baraza la wazazi wa chama cha mapinduzi ccm mayasa kimbau wa pili kutoka kushoto (picha na maktaba)

Katibu wa baraza la wazazi wa chama cha mapinduzi ccm mayasa kimbau amewataka wanaccm kuunganisha nguvu pamoja na kuacha makundi kwa kuwa tayari chama hicho kimemshampata mgombea uraisi ambaye Ni John Pombe Magufuli.

Kimbau aliyasema hayo jana katika kata ya kaloleni wakati akiwanadi wagombea ubunge wa chama cha mapinduzi ccm ambao wapo katika ziara ya kuzunguka katika kata zote za jimbo la arusha mjini ili kunadi sera zao.

Alisema kuwa wapo wanaccm ambao bado hawajavunja makundi kwa kuwa huenda mgombea waliyemtaka hajapitishwa ambapo alisema kuwa chama hicho ni imara katika kufanya uteuzi kwa mgombea nayekubalika.

“Ccm wote sasa ni wamoja tuelekeze Nguvu zetu zote katika kuhakikisha kuwa ccm inacghukua dola na tayari tunae John Pombe Magufuli ambaye anatosha kupeperusha bendera ya chama cha mapinduzi hivyo basi kwa sasa kazi yetu ni kutafuta kura tu nasi vinginevyo”alisema Kimbau

Katika hatua nyingine kimbau alisema kuwa enzi za chama kubeba watu mizigo zimepita na kuwataka wagombea wote kunsadi sera zao na kufuata taratibu kwa kuwa swala la rushwa halina nafasi kwa sasa.

Alisema wanachoangalia kwa sasa ni kuhakikisha kuwa chama kinapitisha mgombea ambaye anakubalika na wananchi na sio chama ili kuhakikisha kuwa jimbo la Arusha mjini linarudi mikononi mwa ccm.

Post a Comment

0 Comments