Ticker

6/recent/ticker-posts

RAFIKI FC WATWAA UBINGWA KOMBE LA SETHI BENJAMINI.



TIMU  ya Rafiki fc ya wilayani Arumeru   imefanikiwa kutwaa ubingwa wa kombe la Sethi Bewnjamini lililofikia tamati jana (jumapili) baada ya kuwafunga wapinzani wao timu ya  Pande  za home kwa kuwafunga kwa jumla ya penalti 6-5.

Mashindano hayo ya kombe la Seth Benjamin yalianza kutimua vumbi mwezi Julai na kufikia tamati mwezi septemba mwaka huu .

Mabingwa hao wa  Rafiki fc waliweza kukabithibiwa zawadi ikiwemo kombe na kitita cha shilingi laki tano ,huku mshindi wa pili  ikiwaendea timu  ya Pnde za Home kwa kuzawadiwa seti ya jezi na mipira miwili na mshindi wa tatu kuwa ni  Chachyi SC baada ya kuwafunga timu  ya Dulluti kwa jumla ya mabao 3-2.

Jumla ya timu 14 kutoka wilaya ya Arumeru zilionyesha ushindani wa aina yake katika kuwania kombe la Seth Benjamini  aliyekuwa muasisi  wa Azimio la Arusha  ambaye alifariki mwaka 1967.

Timu hizo ni  ST.Domingo , Manyata, Duluti,Rafiki, Railway SC, Maji ya chai, Embaseni,Usa Star,Meru Worrious, Pande za home ,Chemchem, Magadini ,Waya  mkali na Chackyi SC zinachuana vikali katika mashindano hayo) yalifanyika katika viwanja vya Ngaresero  ambavyo hizi sasa vinajulikana kama viwanja vya kumbukumbu ya  Seth Benjamini .

Akisoma Risala kwa mgeni rasmi,Mratibu wa mashindano hayo Moody Hassan Orondi, alisema hayati Sethi Benjami ni alikuwa miongoni mwa mashujaa ambao wataendelea kukumbukwa kwani alikuwa ni mmoja wa shujaa aliyeunga mkono azimio la Arusha  kwa matembezi ya miguu.

“Kwa kweli tutamkumbuka sana kwani alikuwa shujaa aliyeonyesha uzalendo mkubwa  kwa kupiga vita Rushwa ,ufisadi, ambavyo hadi leo  ni tatizo katika nchi yetu  hivyo tutaendelea kuadhimisha kkila mwaka na pia uwanja huu tumeupa heshima kwa kuuita  uwanja wa kumbukumbu wa Seth Benjamini”alisema Orondi .
 
Orondi aliongeza kuwa Kwa mara ya kwanza  mashindano hayo yamefanyika ili kuweza kumkumbuka mwasisi huyo ambaye  anakumbukwa kama shujaa ,alikuwa akisafiri kutoka Arusha kwa matembezi  kuelekea Dar es salaam ambapo  alipofika eneo la maji ya chai ,Usa river alizidiwa gafla na kupoteza mwezi julai mwaka 1967.

Mgeni rasmi  katika michuano hiyo Inspector Charles Mbawala ambaye ni makamo  mkuu wa upelelezi wilaya ya Arumeru aliwasihi vijana waendelee kuipenda michezo kwani itawafanya wajijengee mazingira mazuri ya kukuza vipaji  vyao  na kusema jeshi la polisi wilyani  Arumeru linaandaa mashindano ambayo yatashirikisha timu mbalimbali za mpira wa soka.

Mashindano hayo yaliandaliwa na familia ya marehemu kwa kushirikiana na diwani anayemaliza mda wake wa kata ya Usa RIVER (CCM) Zubery Simbano

Post a Comment

0 Comments