Ticker

6/recent/ticker-posts

DONGO JAJA RUKSA KUJIUNGA NA WEUSI :MADII AFUNGUKA RASMI


Ni baada ya show ya Fiesta Dar es Salaam ndipo Nikki wa Pili alisikika akimmwagia sifa kibao Abdul Kachaa almaarufu kama Dogo Janja na kudai kuwa ndiye msanii wake bora wa mwaka.
Yalisikika mengi kwa upande wa Weusi pamoja na Dogo Janja ikiwemo issue ya kufanya kazi pamoja na vitu kama hivyo lakini Madee Ali ambaye ndiye mlezi wa Dogo Janja alikuwa hajasikika kokote kuhusiana na suala hilo.
 imemtafuta raisi wa manzese Madee na kupiga nae story kuwa analizungumzia vipi suala hilo la Dogo Janja kufanya kazi na Weusi, na Madee alikuwa na haya ya kusema.
“Hiyo ni biashara ambayo iko kwenye engo ningine kabisa, kama Dogo Janja ataamua yeye kama yeye mimi wala sitokuwa na shida kwasababu anaweza kuwa anaona kule kuna kitu ambacho atakuwa anakipata tofauti na huku ambako ameishi, me nadhani ntampa uhuru tu na kumtakia mafanikio mema. Lakini kama ni biashara nyingine ambayo hao anaotaka kufanya nao biashara watataka kufanya na Dogo Janja basi itabidi waufuate uongozi wa Tiptop Connection.”
Hayo ni baadhi tu ya maneno ambayo Madee ameyazungumza kuhusu dili hilo la Dogo Janja na Weusi, Play hii video hapa chini kumsikiliza Madee akifunguka juu ya hilo.

Post a Comment

0 Comments