Ni
baada ya show ya Fiesta Dar es Salaam ndipo Nikki wa Pili alisikika
akimmwagia sifa kibao Abdul Kachaa almaarufu kama Dogo Janja na kudai
kuwa ndiye msanii wake bora wa mwaka.
Yalisikika
mengi kwa upande wa Weusi pamoja na Dogo Janja ikiwemo issue ya kufanya
kazi pamoja na vitu kama hivyo lakini Madee Ali ambaye ndiye mlezi wa
Dogo Janja alikuwa hajasikika kokote kuhusiana na suala hilo.
imemtafuta
raisi wa manzese Madee na kupiga nae story kuwa analizungumzia vipi
suala hilo la Dogo Janja kufanya kazi na Weusi, na Madee alikuwa na haya
ya kusema.
“Hiyo
ni biashara ambayo iko kwenye engo ningine kabisa, kama Dogo Janja
ataamua yeye kama yeye mimi wala sitokuwa na shida kwasababu anaweza
kuwa anaona kule kuna kitu ambacho atakuwa anakipata tofauti na huku
ambako ameishi, me nadhani ntampa uhuru tu na kumtakia mafanikio mema.
Lakini kama ni biashara nyingine ambayo hao anaotaka kufanya nao
biashara watataka kufanya na Dogo Janja basi itabidi waufuate uongozi wa
Tiptop Connection.”
Hayo
ni baadhi tu ya maneno ambayo Madee ameyazungumza kuhusu dili hilo la
Dogo Janja na Weusi, Play hii video hapa chini kumsikiliza Madee
akifunguka juu ya hilo.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia