Donald Trump amemshinda Hillary Clinton katika matokeo ya uchaguzi wa urais uliokuwa na ushindani mkali.
Donald Trump amemshinda Hillary Clinton katika matokeo ya uchaguzi wa urais uliokuwa na ushindani mkali.
Bi Clinton amempigia simu Bw Trump kumpongeza kwa ushindi wake.
Rais Obama pia amempigia simu kumpongeza na kutangaza kwamba amemwalika
ikulu ya White House siku ya Alhamisi washauriane kuhusu shughuli ya
mpito.
Bw Trump, aliyeeleza nia yake ya kuwafanyia kazi Wamarekani
wote atakapoingia madarakani, ataapishwa kuwa rais tarehe 20 Januari
mwaka 2017.
Mgombea huyo wa Republican, alishangaza wengi kwa kushinda majimbo mengi muhimu na kujiweka katika nafasi nzuri ya kushinda.
Alishinda majimbo ya Ohio, Florida, na North Carolina, ingawa Bi Clinton alishinda Virginia.
Bw
Trump alijizolea kura 278 za wajumbe na Clinton 218 kwa mujibu wa
makadirio ya ABC News. Mshindi anahitaji kura 270 za wajumbe.
Bw
Trump alishinda majimbo mengi ya kusini mwa Marekani naye Bi Clinton
akashinda majimbo ya kaskazini mashariki mwa nchi hiyo, kwa mujibu wa
makadirio ya shirika la utangazaji la ABC News.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia