Mbunge wa jimbo la Rufuji Mohamed Mchengerwa wa katikati akiangalia baadhi ya bidhaa zinazozalishwa na umoja wa kinamama wa Rufuji. |
Wakinana wakifurahi kwa kucheza wakati wa uzinduzi wa Vicoba Endelevu katika jimbo la Rufiji zoezi liloongozwa na Mbunge wa Jimbo Hilo Mohamed Mchengerwa hayupo pichani. |
MBUNGE
wa Rufiji,Mohamed Mchengerwa (CCM),amesema atapambana na ufisadi
unaofanywa na watu wasio waaminifu katika vikundi vya kuweka na kukopa
vilivyopo katika jimbo hilo,kuhakikisha fedha zinazopatikana zinatumika
kwa matumizi sahihi.
Mchengerwa
alisema hiyo ni njia ya kumuunga mkono rais John Magufuli ambaye
anapingana na ufisadi kila kukicha na anachukia watu wajanja wajanja
wanaojipatia fedha kwa njia za udanganyifu.
Mbunge
huyo alitoa kauli hiyo jana wakati wa uzinduzi wa vikoba endelevu
ambavyo vimejumuisha vikundi tisa ambapo hadi sasa akiba Zaidi ya
milioni 45.
‘’Pamoja
na jitihada hizi za kuhakikisha tunajikwamua na umasikini kwa kujiunga
katika vikundi ili tuweze kusaidiana kirahisi bado kuna watu ambao
wanafanya ufisadi ili kuviua vikundi,nitakwenda kushughulika nao wote
ikiwa ni njia ya kumuunga mkono rais wetu John Magufuli ambaye kila
kukicha anapingana na mafisadi’’
Mchengerwa
ambaye baada ya uzinduzi wa vikoba hivyo alichangia shilingi 6,500,000
na kuahidi kutoa milioni mbili zingine aliwataka wanavikundi hivyo
kuhakikisha kuwa fedha hizo zinatumika katika maendeleo na kuonya wenye
mtindo wa kugawana fedha zinapotolewa.
‘’Naomba
fedha hizi zitumike katika matumizi sahihi,nakumbuka hivi karibuni
nilitoa pikipiki katika vikundi lakini taarifa zilizopo ni kwamba watu
wameenda kuuza na kugawana fedha jambo ambalo si sahihi,tunajirudisha
nyuma wenyewe’’alisema Mchengerwa
Alisema
wananchi wa Rufiji ni masikini na wapo nyuma kimaendeleo hivyo ni
jukumu la kila mmoja kuhakikisha anakuwa mstari wa mbele kuukataa
umasikini huo kwa vitendo.
‘’Nimejitolea
kusaidia watu wa Rufiji kwa kuwa mlinichagua ili niwawakilishe,naombeni
kila mmoja aguswe na umasikini tulionao na awe na dhamira ya dhati ya
kuutokomeza,vikundi hivio vitumike vizuri mkopeshane muweze kuendesha na
kuanzisha biashara zenu,naahidi kuwa bega kwa bega na nyie na leo hii
(juzi) nawakabidhi mke wangu Farida Mchengerwa kuwa mlezi wenu ili
msaidiane’’alisema Mchengerwa
Kwa
upande wa mlezi wa vikundi hivyo,Farida Mchengerwa,aliwataka wananchi
kutumia fursa hiyo kujiunga na vikundi hivyo ili waweze kukopesheka
kwani inajulikana kuwa masikini hakopesheki kutokana na masharti
yanayowekwa na taasisi za fedha ambayo wengi hawana uwezo wa kuyamudu.
Akizungumza
kwa niaba ya wanavikundi hivyo,Abdulrahman Hafidh,alisema vikundi hivyo
kwa sasa vina wanachama zaidi ya 220,kutaja changamoto zinazowakabili
kuwa ni pamoja na uelewa mdogo wa wanavikundi kuhusu vicoba endelevu
jambo ambalo Mchengerwa aliahidi kulishughulikia kwa kumuwezesha mwalimu
ili aendelee kuwapa elimu.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia