MAHAKAMA YA BARAZA LA NYUMBA LATEMBELEA ENEO LENYE MGOGORO WA SHAMBA

MAHAKAMA ya baraza la ardhi na nyumba wilayani Arusha mwishoni mwa wiki iliyopita lililazimika kuendeshea kesi yake nje ya mahakama hiyo baada ya kutembelea eneo la mgogoro wa shamba  lililopo katika kijiji cha Sakila wilayani Arumeru mkoani Arusha.

Hatua hiyo ilifuatia baada ya shauri nambari 35 la mwaka 2005 lililofunguliwa mahakamani hapo na mdai,Augustino Nko dhidi ya kanisa la International Evangalisim Church ambapo anadaia kuporwa ardhi na kanisa hilo kwa kuingilia mipaka ya shamba lake.

Hatahivyo,malumbano makali yaliibuka wakati wa kufika katika eneo la tukio ambapo ilimlazimu mwenyekiti wa baraza hilo,Dorith Mangure kuamuru eneo lenye mgogoro lipimwe ukubwa wake sanjari na mipaka yote ili kuondoa utata.

Akizungumza kabla ya zoezi la kukagua na kupima mipaka ya eneo hilo,Mangure alisema kwamba  lengo kuu la baraza lao kufika kijijini hapo ilikuwa ni kupima ukubwa wa eneo hilo sanjari na mipaka yote iliyopo katika eneo hilo ili kujiridhisha zaidi.

Hali hiyo iliwalazimu baadhi ya watumishi wa baraza hilo kumwapisha kwa kiapo shahidi  kutoka upande wa washtakiwa,Ndewario Isangywa  kwa  lengo  la kuonnyesha ukubwa na mipaka ya eneo hilo baada ya shahidi wa kwanza,Elisa Nko kukataliwa na upande wa walalamikaji.

Mara baada ya kukamilsha zoezi  la upimaji huo,Mangure alisema kwamba eneo hilo lina ukubwa wa ekari 2.3 ambapo upande wa kusini linapakana na familia ya Robert  Meshack,upande wa kazkazini  linapakana na chuo cha bibilia cha kanisa la IEC,upande wa mashariki linapakana na familia ya Winston Nko na upande wa magharibi linapakana na familia ya marehemu mzee Meshack Nko.

Mara baada ya kufafanua vipimo hivyo alisema kwamba baraza lao limekusanya ushahidi mbalimbali ambapo uitawasilishwa kwa jaji wa mahakama hiyo kwa lengo la kupanga tarehe ya kutoa uamuzi kuhusiana na  sakata hilo.

Akizungumza mara baada ya zoezi hilo wakili upande wa  walalamikaji ,Duncan Oola alisema kwamba mteja wake alifungua kesi mbele ya baraza hilo kulalamikia kitendo cha kanisa hilo kuingilia eneo lake na ndio sababu iliyopelekea baraza hilo kutembelea eneo hilo.

Oola,alisema kwamba mteja wake alifungua kesi  mbele ya baraza hilo mwaka 2005 na kisha kushindwa mwaka 2007  hatahivyo  alikata rufaa mwaka huo huo kwa kile alichodai ya kwamba hakuridhika na uamuzi wa baraza hilo.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia