SEREKALI YATAKIWA KUTOA TAMKO LA WATU WAVURUGAO AMANI

UMOJA wa makanisa Arusha na Kanda ya Kaskazini umesema kuwa kitendo cha serikali kutoyakuchukulia hatua makundi yanayoendesha harakati za kuvuruga amani nchini kinaonyesha kuwa serikali inakubaliana nayo.

Hayo yalisemwa jumanne na askofu Joseph Mutorela wa kanisa la Monnonite Tanzania alipokuwa akisoma tamko la pamoja la umoja huo kwenye hoteli ya Corridor Spring kwenye kikao kilichoudhuriwa na askofu wa KKKT, dayosisi ya kaskazini kati, Thomas Laizer, Msaidizi wa askofu wa kanisa la katoliki jimbo kuu Arusha,  Simon Tenges, askofu wa Anglikana daiyosisi ya mlima Kilimanjaro, Stanley Hotay pamoja na wawakilishi toka madhehebu ya kipentekoste.

Alisema kuwa kwa nyakati tofauti baadhi ya waislam kupitia mihadhara na  vyombo vya habari wamekuwa wakitoa maneno ya uchochezi na kashfa dhidi ya ukristo pamoja na kueneza chuki katika jamii lakini serikali imekuwa haichukui hatua zozote kudhibiti hali hiyo isiendelee.

“Kwamba hali ya uchochezi na vitisho imeenda mbali zaidi hadi kuingia katika uharibifu wa mali na kusitisha uhai wa watu wa Mungu, mfano uchomaji wa makanisa na uharibifu wa mali Zanzibar mnamo tarehe 26, 27 na 28 may, 2012 na kifo cha mwinjilisti huko Mto wa Mbu februari 24, 2011”

“Wajibu wa Serikali kusimamia sheria na taratibu za nchi. Hivyo inapoonekana baadhi ya makundi yakiendelea na harakati zao za kuvuruga amani na kusababisha hofu bila hatua zozote madhubuti kuchukuliwa kunaleta hisia kuwa baadhi ya viongozi wa Serikali wanakubaliana na hali hiyo” alisema Askofu Mutorela.

Aidha alidai kuwa kuwa ukimya wa kistaarabu ambao umeendelea kuonyeshwa na wakristo kwa jinsi yoyote usitafsiriwe kama ujinga wala uoga ambapo aliwataka Wakristo wote nchini kumuomba Mungu aliye hai ili kusudi lake likasimame.

Hata hivyo viongozi hao wa dini hawakukubali kutoa fursa ya kuulizwa maswali na wanahabari waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano huo kwa madai kuwa kwenye ratiba ya hawakupanga kipengele hicho.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia